Alikufa kwa Ngoma...(ila hakuonekana na binti)

For all the incognito Team DRYFRY members…this song is about you

https://www.youtube.com/watch?v=XRraufg7Mzw

Verse 1

Hakuonekana na binti hakuwahi kuiasi dini

Mfuasi mzuri wa maadili lakini alikufa kwa ngoma

Aliwarudisha waliopotea akawapa tiba mbadala

Na adui mkubwa wa zinaa lakini alikufa kwa ngoma

Najaribu kumjengea picha mshkaji alie kalala ndani ya futi 6

Namkumbuka mtaani mtaani alipokuwa anakatisha

Na mara kadhaa maskani washkaji ungemkuta

Usingedhani ana ngoma machoni alivyokuwa mwema (alivyokuwa mwema)

Mzuri, mtanashati aliyewaza kabla ya kusema

Ibilisi wa njaa za mwili daima alimchezea mbali

Tungi, vicheche, mineli hakuonekana kujali

Tazama maisha yake hutaliona kosa lake

Kama aliyefunga kufuli kati kati ya nyeti zake

Mkali wa ushauri nasaha aliyeongea kuhusu mapenzi huku akipinga zinaa

Ungesema achague kipindi angechagua njia panda

Nyumba aipendayo angechagua ya ibada

Utepe mwekundu mpaka kwenye nguo zake za ndani

Nadhani mimi najali wewe je?

Kama alikufa kwa ngoma jiulize alijali nini!

Kiitikio (chorus)

Hakuonekana na binti hakuwahi kuiasi dini

Mfuasi wa maadili (Lakini alikufa kwa ngoma)

Alirudisha waliopotea akwapa tiba mbadala

Adui wa zinaa (lakini alikufa kwa ngoma)

Verse 2

Mara nyingi alikuwa mpole mara chache alizoongea wote tulimgeuza shule

Nasaha za bure kama tupo class vile akatuasa kuhusu kuhusiana

Akatuonya kutoaminiana mtazamo wake na wa-mama Terry daima ulifanana

Hadithi ya maisha yake ilikuwa safi kama ya Nabii

Hakuna aliyeamini mwisho wa mshkaji utakuwa namna hii

'Gawa sana condom na kufunza kama angaza

Vijarida vya Ukimwi ye’ndio alikuwa msambaza

Ina maana alikuwa anatoa bila vyake kubakiza

Ama amekuwa ufunuo mola anaonyesha miujiza

Tazama siku zinakata hatumuoni nini kasoro

Afya yake haieleweki eti imeanzisha mgogoro

Leo anadunda kesho mgonjwa na hataliacha godoro

Labda alifanya kwa siri hadharani hakuna shahidi

Labda alivumilia sana mwisho kuasi kukambidi

Hatujui! hatuwezi sema na bado tunashangaa

Vipi vipimo vinasoma mshkaji alikufa kwa ngoma

Kiitikio

Hakuonekana na binti hakuwahi kuiasi dini

Mfuasi wa maadili (Lakini alikufa kwa ngoma)

Alirudisha waliopotea akwapa tiba mbadala

Adui wa zinaa (lakini alikufa kwa ngoma)

Verse 3

Sijaribu kuibadili nyekundu kuwa njano huu ni mfano

Kwamba Ukimwi ni kwa wote wembamba na wacheza sumo

Wazinzi, wema pia wamo na hauji kufuata kimo

Ungedhani yupo salama kuzidi usalama wenyewe

Ungedhani ukimwi utaogopa utamuacha mshkaji mwenyewe

Sivyo! Haufanyi utakavyo wewe unafanya utakavyo wenyewe

Hakuonekana ana binti hakuwahi kuiahasi dini

Mfuasi mzuri wa maadili “Lakini alikufa kwa ngoma”

Amsha akili janga kangha gani ulibebebee

Siwaambii msiusie sisemi zipu mfungue

Sisemi muache kuwa wema ila ujinga usiendelee

Kwamba kila anayekufa kwa ngoma msidhani kicheche

Tuamini bado ni wenzetu msiache wagonjwa wajifiche

Kiitikio

Au sio, tumeelewana naamini, tusihukumu

Hatuna hakina kuwa waathirika wana hatia

Tusiwanyenyepaee…aaight!?

© Mwana FA

I hate that song… Makes me feel ka niko nayo

huyo ni Mwana FA

Kama hakuonekana na binti? Alikuwa akionekana na majamaa!
Hii song ni jui ya ma downlow brothers, ma father wa catholic and the rest.

1 Like

lady jaydee enyewe ametoka mbali

Nice song.

You should listen to “Mdananda” by Shetta, Tundaman and Dully sykes. It’s about a dude who was set up to DFHKM a HIV positive lady in exchange for money.

https://www.youtube.com/watch?v=uQFQDumaBLI

feeroz na professor jay …kwaherini.

5 Likes

ukishapatikana nayo…sikiza hii ya daz nundaz family…kamanda.

https://www.youtube.com/watch?v=mrxFySY45wc

3 Likes

Hahahahahaha you guys are crazy …Tanzanians are great composers

1 Like

Ilikua huzuni kwa ndugu na wasela…blabla, Alazwe pema huyo

the song was about bum drillers and drillees and how hiv was sweeping them

@Web Dev I DEDICATE THIS THREAD TO YOU AND @junkie

Wakameat we have a cease fire, whose your new boyfie!

https://www.youtube.com/watch?v=k3DvU8iWdyQ

i dont like it