Anaomba ushauri kachanganyikiwa

Iko hv kuna dogo anamchumba wake

mwanaume anakaz nzuri kiasi ila ukoo mzima unamtegemea yeye uko kijijini baba ake anawake 3 ambapo asilimia 80% wanamtegemea jamaa kuanzia chakula kila kitu

Sasa jamaa kumbe alimpenda bidada kwakumuona anaroho nzuri pia anakibiashara kidogo ambacho kinatosha …so lengo la jamaa nikwamba wasaidizane na bidada kuwainua familia yake kiuchumi
Sasa ugomvi unakuja maana bidada anandoto za kua na maisha mazuri angalau aweze kuishi vizuri ,wakati jamaa anania ya kuwainua kwao ikiwemo kuwasomesha kuwajengea

Bidada kaniomba ushauri anashindwa aamue nini sababu jamaa jana kamuambia hela yake yeye anajenga na kufanya maendeleo kwao hela ya bidada inabidi atumie kwa ajiri ya kufanya maendeleo,kununua vitu vya ndani yeye atakua anamsaidia kidogokidogo,

Bidada anaona kama nimtihani mzito sababu hata mahitaji yake binafsi jamaa hayafanyi juz wameenda shopping mdada kanunuliwa kiatu cha elf 10 tu wakati jamaa katumia laki 3 kununua nguo na viatu vya ndugu zake

Yupo njiapanda afanyeje wazazi wa

Ndugu wamekuwa wakiua mahusiano mengi na kuleta migogoro kwasababu ya utegemezi…

Familia nyingi za kiafrica bado ni tegemezi kwa ndugu zao…hivyo huyo bidada avumilie tu

Hakuna ndoa hapo tena, aondoke tu afanye yake, mwanamme wa wapi kwani huyo Mbona mshamba sana

Mwambie bidada ukipenda boga apende na ua lake

Mwanaume sio mshamba, inaonekana bidada hakukaa na jamaa kuzungumza chakufanya wakae wazungumze kwanza na bidada atoe dukuduku lake mapema

Wazazi wanashindwa kutengeneza maisha yao wanakuja kusumbua watoto mbelen we MTU hauna uwezo wanawake 3 wanini?

Kweli kuliko kujifanya anakubaliana nae huku moyoni anaumia

Yaani asikae nalo rohoni kabisa maana baadae litaleta shida, wakae wazungumze tena mapema

Sawa ampe muda waongee ikishindikana asepe, hata hivyo lakini mwanamme mshamba

Inawezekana anaogopa ataonekana hapend ndugu wa mume

Hahaha sio mshamba hizo ndo familia nyingi za kitanzania zilivyo. Sasa kuna nyingine mwanaume anaoa mke ambae na anahudumia familia ya mkewe pamoja na yake

aamue tu mapema asije akajuta uko mbeleni

Yes na ataonekana hivyo hivyo na kama wakwe wakisikia ilo suala basi ndoa haina future hiyo

Kama ndo wewe ungeamuaje? Mbona kuna wanaume wanasaidia familia ya mke hili suala kwa mwanamke mwenye akili haliwezi vunja ndoa/mahusiano yake na mumewe

Mmh pagumu hapo

kama aliambiwa tangu mwanzo akakubali bas apambane tu bt kama hakuambiwa huyo ME aache usoro aangalie kotekote.!

kama ni mm tungekaa tuongee mapema kabla hatujafika mbali swala la kusaidia ndugu sio shidaa …je anatoa huduma ya familia? kama hatoi ananiachia mm pekee hapa sitaelewaa
kama anabalance kote ni sawa tunasogeza maisha sabbu familia zetu za kitz ndo hvyo

Pole yake hiyo mdada ndio familia zetu za kiswahili hizo hapo bado hajaolewa mwambie afanye maamuzi kabla hajaingia kwenye ndoa

Familia nyingi za kiafrika zikikusomesha ujue wewe ndiobunakuwa nguzo ya kuinuia ukoo mzima huyo mwanamke aachane nae huyo mgongo wa ukoo atamchelewesha sna maana hataki kuwasaidia wazazI ili wasiwe tegemezi kwake yeye anataka kuwabeba muda waote

Hakuna mume hapo