[SIZE=7]Taarifa kutekwa tajiri kada wa CCM zazua taharuki[/SIZE]
http://www.mwananchi.co.tz/image/view/-/4639504/highRes/2027930/-/maxw/600/-/11wag8d/-/ZACHARIA+PIC.jpg
Mfanyabiashara maarufu na kada wa CCM, wilayani Tarime, Peter Zakaria.
[SIZE=5]Kwa ufupi[/SIZE]
Zakaria, ni mmiliki wa mabasi ya Zakaria yanayofanya safari za Musoma, Tarime kwenda maeneo mbalimbali nchini.
By Waandishi Wetu, Mwananchi [email protected]
Tarime/Musoma. Taarifa za kutoweka kwa Mfanyabiashara maarufu na kada wa CCM, wilayani Tarime, Peter Zakaria zimezua taharuki kwa wakazi wa mji huo.
Zakaria, ni mmiliki wa mabasi ya Zakaria yanayofanya safari za Musoma, Tarime kwenda maeneo mbalimbali nchini.
Awali, leo Juni 30 zilizagaa taarifa kuwa mfanyabiashara huyo ametekwa na akapatikana kisha akapelekwa hospitali ya Wilaya ya Tarime kwa matibabu.
Baada ya taarifa hizo, wakazi wa mji huo walimiminika hospitalini hapo kwa nia ya kutaka kuthibitisha kama yupo au la lakini jeshi la polisi lilifyatua mabomu ya machozi kuwatawanya.
Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Glorius Luoga amesema hawezi kuzungumzia tukio hilo hadi Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Tarime/Rorya atakapotoa taarifa rasmi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Polisi Tarime/Rorya, Heny Mwaibambe amesema mfanyabiashara huyo hakutekwa bali anashikiliwa kwa mahojiano lakini hakutaka kuzungumzia kwa undani suala hilo.
Kabla ya matukio haya, jana Juni 29 ilisikika milio ya risasi katika kituo cha mafuta cha mfanyabiashara huyo kilichopo Tarime mjini.
Tutaendelea kuwapa taarifa zaidi za tukio hili.
ITV Tanzania
1 hr ·
#HABARIZILIZOTUFIKIA:Mmiliki wa Mabasi ya Zacharia Bw Peter Zacharia anashikiliwa na vyombo vya dola mkoani Mara kwa tuhuma za kuwapiga risasi maafisa wa idara ya Usalama wa Taifa wakiwa katika majukumu yao.
Taarifa zaidi kukujia endelea kuwa nasi.
https://scontent-mrs1-1.xx.fbcdn.net/v/t1.0-0/p526x296/36450356_1620874854690149_8081204305723392000_n.png?_nc_cat=0&oh=893325dbc34af145a62d5edc3bd365f4&oe=5BEB8E19
RadioOneStereo
20 mins ·
Kufuatia tukio la Maafisa wawili wa Idara ya usalama wa Taifa kujeruhiwa kwa kupigwa risasi na mmiliki wa mabasi ya Zacharia mjini Tarime, Mwanahabari wetu #GeorgeMarato anatusimulia kwa kina kilichojiri huko.
https://scontent-mrs1-1.xx.fbcdn.net/v/t15.0-10/30833743_736119873430527_2151087194280820736_n.jpg?_nc_cat=0&oh=2320e762210e56d35faa6a8ff35c7891&oe=5BA1B29D
Pause
-1:54
Additional Visual Settings
Enter Watch And Scroll