Eid na Vituko vyake!!

Habari za ugenini?
Niende kwenye mada:
Kama mjuavyo kesho ndio sikukuu ya Eid
Nimeshuhudia ugomvi kati ya wake na waume zao baada ya wanaume wengi kushindwa kumudu/kukidhi mahitaji ya familia zao ikiwemo kununulia nguo watoto,viatu na chakula cha sikukuu.
Baadhi ya wanawake wamewakunja na kuwapiga waume zao,wengine wamewanunia na wengine wakakataa hata kutoa chakula cha usiku “papuchi”
Najiuliza hawaoni vyuma vimebana na mambo yamebadikika,hata sisi wengine tunapost mada zetu tukiwa kwenye server za ugenini?
Wanawake please and please mtuhurumie,maisha ni magumu kwa wengi wetu.
Eid Mubarak

Nawasilisha!

eeeh bwana hili la nguo za watoto kidogoo liniletee shida… sema nikampigia jamaa yangu kumkopa ndo akanikumbusha kwamba namdai wazfa mrefuuu… kapunguza deni ndo ikawa pona yangu

kumbe nimekua wa kwanza kukomenti,… hahaha

Kuna kipind kimoja nilikua nasikiliza kila jionbaada ya ftari, kinasema siku za mwisho wa mwezi wa ramadhan wanandoa au wazazi wanakua na ugomv wanawake wakiongoza

Hivi unajua na kuona kabisa mumeo hana pesa, akaibe? Ifikie hatua tutambue kuna kupata na kukosa s kila siku mtu atapata tu

Hahaha, Ati na wewe umecome kwa huku…

Eeh mkimbizi

Asubuhi njema my dada

Na kwako pia

Hulali?

Nalala

Bas Sawa

Hizo nguo za sikukuu zitatukosesha ndoa haki ya mzungu.

kama mumeo hana pesa njoo kwangu

Mkuu watu kuachana wewe unasema vituko

Kuachana kwangu ni kituko,maana baada ya muda si mrefu wanarudiana!

Aisee! Sikukuu ilikuwa poa sana
Nalog off

Hahahahaha

Maisha haya jamani

Eid haiji kwa bahati mbaya,siku zote maisha ni mipango.Lazima tuwe na nidhamu ya kuweka akiba kila wakati kulingana na kipato chetu ili kuweza kumudu matumizi yetu kwa uhakika bila masikitiko na stress

MAtayarisho ya Sikukuu ya Eid yalianza tangu tarehe 17/05/2018.

So, why kulalama nakujipa sababu kibao ya kushindwa kutimiza jukumu lako.
Tuenge tabia ya kuwa na financial discipline