FADHLA ZA SIKU KUMI ZA MWEZI WA MFUNGO TATU

Mwenyezi Mungu Alipomuumba mwanadamu ili aje afanye ibada na Akaumba Pepo na Moto, kwa mwenye kutwii na mwenye kuasi. Akawawekea misimu ya ibada nyakati mbalimbali ili wazidishe thawabu waingie peponi kwa usahali.
Allah Anaumba na Kuchagua
Ama baada ya kumshukuru Allah (Subhaanahu wa Taala). Enyi Waislamu muogopeni Allah Ambaye Anaumba na kuchagua, kwa mfano ameumba mbingu na Ardhi na akajichagulia mbingu ya saba na Makka pakawa ni patakatifu akaumba pepo na Malaika, akaifanya firdausi ndio pepo ya juu zaidi, na Jibril ndiye kiongozi wa Malaika na katika mwaka akaweka miezi, siku, nyakati za siku na saa. Akachagua mwezi mtukufu wa Ramadhani, siku bora ni Ijumaa, usiku mtakatifu ni Lailatul Qadri, na saa ya kukubaliwa dua ipo Ijumaa na masiku matukufu yapo kwenye siku kumi za mwanzo wa mfungo tatu. Allah akawaumba wanadamu, akawachagua aliowathamini ni muuminina, na akawachagua katika muuminina mitume, akawapandisha cheo mitume fulani, akaita rusul, na katika rusul akawapandisha wengine wanajulikana ulul–‘azm, na katika hao akatubainishia vipenzi vyake, na bila shaka katika vipenzi vya Allah kiongozi wao ni Mtume wetu Muhammad (Swalla Llahu ‘alayhi wasallam).
https://www.islamkingdom.com/sw/fadhla-za-siku-kumi-za-mwezi-wa-mfungo-tatu

just don’t blow us up while you are at it…