Holy Gospel of Jesus Christ according to Saint Luke 1: 57-66

Wakati wa kujifungua kwake Elisabeti ulifika, akajifungua mtoto wa kiume.

Jirani na watu wa jamaa yake walipopata habari kwamba Bwana amemwonea huruma kubwa, walifurahi pamoja naye.

Halafu siku ya nane walifika kumtahiri mtoto, wakataka kumpa jina la baba yake, Zakaria.

Lakini mama yake akasema, “Sivyo, bali ataitwa Yohane.”

Wakamwambia, “Mbona hakuna yeyote katika ukoo wake mwenye jina hilo?”

Basi, wakamwashiria baba yake wapate kujua alitaka mtoto wake apewe jina gani.

Naye akaomba kibao cha kuandikia, akaandika hivi: “Yohane ndilo jina lake.” Wote wakastaajabu.

Papo hapo, midomo na ulimi wake Zakaria vikafunguliwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.

Hofu ikawaingia jirani wote, na habari hizo zikaenea kila mahali katika milima ya Yudea.

Wote waliosikia mambo hayo, waliyatafakari mioyoni mwao wakisema: “Mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana, hakika nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye.

Hilo ndilo neno la Bwana

Sifa kwake ewe Kristu.

Asante kwa neno, Mungu akubariki

Mungu akubariki pia wewe kaka

Injili ya leo hii!!

y

Mkuu,hichi ni kisa cha kuzaliwa kwa "Yohana Mbatizaji",sasa mbona unamsifu Yesu Kristu…,Yesu(Isa) alitiwa tohara(kytahiriwa/kukatwa govi) siku nane baada ya kuzaliwa,na hichi kisa cha kuzaliwa Yohana mbatizaji naona na yeye alikwatwa “Govi” kama ilivyoandikwa katika Luka:1:59 ."Mtoto alipokuwa na umri wa siku nane, watu wakaja kuhudhuria tohara yake. Wote wakataka wampe yule mtoto jina la Zakaria, yaani jina la baba yake"…,kukata govi ni mila za kiyahudi,Yesu kafanya na wayahudi wote wanafanya mpaka hawa wa leo

Mkuu,swali langu mbona wakristu wa siku hizi hamtiwi tohara…au mnafata Yesu kwa kumuhubiri katika majukwaa tu…Kumbuka yesu kawalaani sana wale wanaomtangaza kwenye majukwaa lakini hawafati yale aliyohubiri… kama Yesu alivyosema katika biblia Matayo 7:21-23

Matayo 7:21-23
“Sio kila mtu anayesema, ‘Bwana, Bwana,’ ambaye ataingia katika Ufalme wa mbinguni(Peponi) ila ni wale wanaofanya mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni(Mungu). 22 Siku ile itakapofika(Mwisho wa dunia) wengi wataniambia, ‘Bwana, Bwana, hatukutoa unabii na kufukuza pepo kwa jina lako; na kufanya miujiza mingi ya ajabu kwa jina lako?’ 23 Ndipo nitawaambia wazi, ‘Siwafahamu kamwe. Ondokeni kwangu nyinyi watenda maovu!"…

Karibu tujadiliane

Very interesting

[SIZE=5]ukafiri bana, unakua punguani hivi hivi unajiona.[/SIZE]

Mkuu ss hatufuati mila za wayahudi…Bali tunaenenda ktk imani yake…ntakupa mfano,kuna wakati watu walimfuata Yesu wakwambia kuwa mama yako na ndugu zako wanakutafuta…akawajibu kuwa mama yake na ndugu zake ni wale waendao ktk njia zake…Pia kuna wakati wayahudi hao hao walimpeleka mwanamke mzinzi kwa Yesu wakitaka wampige mawe afe…hiyo ilikuwa ni mila yao kwa mwanamke kahaba adhabu yake ni kifo…ila Yesu aliwaambia kuwa yeyote asiye na dhambi na awe wa kwanza kutupa jiwe…hakuna aliyethubutu na hatimaye wote waliondoka…ninachotaka nikwambie ni kuwa kutenda hizo tamaduni za kiyahudi sio tiketi ya ww kuingia mbinguni…tiketi pekee itakayokupeleka mbinguni ni matendo yako…That’s why Yesu aliwaita wale mafarisayo wanafiki…

Mkuu,nafikiri itakuwa vigumu kufuata Imani ya Yesu bila ya kufuata mila za Kiyahudi,kwani Yesu kaja kwa ajili ya Wayahudi tu sio kwa ajili ya binadamu wengine hayo kayasema Yesu kwenye Biblia…katika matayo Matayo 15:22-24,katika kisa ambacho Yesu alikataa kumtibu mtoto wa mama aliekuwa sio Myahudi,Yesu aliwambia wanafunzi wake kuwa Yeye katumwa kuja kwa wana wa Israel (Mayahudi)tu;;

Matayo 15:22-24
22 Mwanamke mmoja Mkanaani aliyeishi sehemu hizo akaja kwake, akamlilia, akasema, “Nihurumie, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu amepagawa na pepo na anasumbuka sana.” 23 Lakini Yesu hakumjibu neno. Basi wanafunzi wake wakamwendea wakamwomba, “Mwambie aende zake, kwa maana anaendelea kutupigia kelele. ” 24 Akajibu, “Nimetumwa tu kwa ajili ya kondoo wa Israeli waliopotea.”

Hapa ndo wengi wanapotea… Usichukue neno kama lilivyo katika bible na kulitafsiri hivyohivyo…Bible inasema watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa…ndo maana kuna walimu na wachungaji wakuweza kutafsiri haya maandiko…Israel anayomaanisha Bwana Yesu ni kanisa lake la leo…ndo maana hapo anawaambia wanafunzi wake kuwa ametumwa kwa kondoo wa Israeli waliopotea…ni wakina nani hao waliopotea??? Ni wale wakristo walorudi nyuma ktk dhambi ili awarejeshe tena kundini mwake…Ndugu wayahudi hawakumkubali Yesu wala mafundisho yake…ni hawa hawa walomsurubisha…ndo maana akasema “Nabii hakubaliki kwao”.That’s why Yesu alituagiza tuenende katika imani…Imani yako ndiyo itakayo kuponya…

Mkuu,Hapo ndipo wachungaji wanapowapotosha wafuasi wao,naweza kukwambia kuwa Yesu hakuwahi kujenga kanisa,hamna hata sehemu moja katika biblia Yesu amesema kuwa yale anayoyahubiri yanaitwa dini ya Kikiristo,…Hiyo mistari ya biblia matayo Matayo 15:22-24, niliyokuweka iko wazi kabisa,Kuwa yeye Yesu alikataa kumtibu mtoto wa yule mama kwasababu yule mama na mwanawe walikuwa sio wayahudi,haina haja ya kutafsiriwa na Mchungaji ili uifahamu

Wana wa Isaeli waliopotea ni wale wayahudi waliokuwa hawafati mafunzo ya kitabu cha “Taurati”,kulikuwa hakuna Ukiristo wakati huo Yesu hakuhubiri “Ukiristo”,Yesu aliendeleza mafunzo ya kitabu cha Taurati,kitabu cha Musa(Moses)…

Kuna kisa chengine katika biblia Yesu aliwambia wanafunzi wake 12 kuwa wasiende kuhubiri kwenye nyumba ya mtu yeyeyote sipokuwa nyumba za Wayahudi,kwanza yeye mwenyewe alikataa kuwatibu watu walikuwa sio Wayahudi halafu aliwaamrisha wanafunzi wake wafanye hivyo hiyvo….,kama ilivyoelezwa kwenye Matayo 10:1-7

[SIZE=5]Matayo 10:1-7 : Bibilia Takatifu [/SIZE]
Ndipo Yesu akawaita wanafunzi wake kumi na wawili, akawapa mamlaka ya kutoa pepo wachafu na kuponya magonjwa yote na udhaifu wa kila aina. 2 Majina ya hao wanafunzi kumi na wawili ni haya: 3 wa kwanza, Simon, ambaye aliitwa Petro, na Andrea ndugu yake; Yakobo, mwana wa Zebedayo na Yohana ndugu yake; Filipo na Bartholomayo; Tomaso na Mathayo mtoza ushuru; Yakobo mwana wa Alfayo, na Thadayo; 4 Simoni Mkanaani; na Yuda Iskariote ambaye baadaye alimsaliti Yesu. 5 Yesu aliwatuma hawa kumi na wawili(12), akawaagiza, “Msiende kwa watu wa mataifa wala msiingie mji wo wote wa Wasamaria. 6 Bali waendeeni kondoo wa nyumba ya Israeli waliopotea. 7 Na mnapokwenda, hubirini mkisema, ‘Ufalme wa mbinguni umekaribia

Mkuu hii mistari haina haja ya kutafuta mchungaji akutafsirie,labda uwe hujui Kiswahili,Wana wa Israel imekusudiwa Wayahudi,kwa kiarabu wanaitwa “Bani Israel”,Wana wa Israel sio Wakristo kama unavyosema wewe,usipotoshe maana na ujumbe aliokuja nao Yesu kwa binadamu