I'M SORRY BASATA; 219 YA SUGU NI NGOMA KALI

I’M SORRY BASATA; 219 YA SUGU NI NGOMA KALI

Wiki iliyopita nilipata bahati ya kusikiliza ngoma mpya ya Sugu inayotambaa kwa jina 219. Niliposikiliza kigongo hicho, baadaye nikasikia Baraza la Sanaa la Taifa (Basata), limeupiga ‘loki’ wimbo huo.

Nina mambo mawili ya kuzungumza; kwanza ni kuhusu wimbo na maudhui yake, pili ni Basata na uamuzi wake.

KUHUSU MAUDHUI

219 ni namba ya Sugu ambayo alipewa jela kama utambulisho wake. Kuhusu Sugu kuwa jela na sababu ya kufungwa siyo jambo lenye kuhitaji maelezo. Kila Mbongo anajua. Jumuiya za Kimataifa zinajua, wewe Mtanzania usijue kwa upofu na ukiziwi upi? Anyways, kama hujui muulize jirani yako, maana habari anayo!

Basi 219 Sugu amefanya ndio jina la wimbo. Ni ngoma kali. Credit kwa prodyuza Mr T Touch kwa uchakataji alioufanya ndani ya ‘kiwanda’ chake cha “Touchez Sound”, ila makofi mengi kwa Sugu a.k.a Jongwe kwa kazi nzuri; flaws zenye mamlaka ya kidingi kwenye game, ameitendea haki topic aliyoikusudia, kuhusu vina (rhymes), Baba Sasha-Desderia amenyoosha mbaya.

Bonge la chorus. “Mfungwa wa kisiasa 219, najua Mbeya ndio inanitesa. Lakini bado napenda Mbeya inavyonitesa.”

Ukiusikiliza wimbo unapata picha jinsi ambavyo Sugu alivyochukulia kifungo chake kwa tabasamu na kukigeuza mtaji kwa jamii yake ya Mbeya ambayo humwita Rais wa Mbeya. Mwaka 2020 ikiwa Sugu atagombea tena ubunge, hatatakiwa kuongea sana, akiweka tu mdude 219, anawarusha wapigakura, kura nyingi kwake.

Sijasikia tusi wala lugha yenye kuudhi kwenye wimbo. Je, labda ni aliposema wanataka kumshuti kama Lissu? Au alipohoji mbona Akwilina alipigwa risasi na kufa wakati hakusema chochote? Au alivyosema amefungwa bila kosa? Yaani kweli Basata walitaka Sugu afungwe halafu aseme alifungwa kihalali?

TUWAAMBIE BASATA

219 ni wimbo usio na kasoro yoyote. Tamko la Sugu kwamba atawapeleka mahakamani naliunga mkono. Mnafungiaje wimbo wa mtu ambao umekidhi vigezo vyote vya kisanii?

Basata mwache kutabirika. Wimbo hauna kasoro yoyote. Labda ni kutekekeleza agizo kutoka juu. Na hili Sugu amelisema kwenye wimbo: “mnamfunga mbunge bila kosa, matokeo yake wao ndio usingizi wanakosa.”

Sugu ni mwanamuziki. Hisia zake ataziweka kwenye muziki. Kama Papii Kocha alivyotoa “Waambie” baada ya kutoka jela au FM Academia ya Ndanda Kosovo walivyotoa Jela, ndivyo Sugu alivyotoa 219. Kumfunga ni sawa, lakini huwezi kumpangia namna ya kupokea na kuwasilisha hisia zake za kufungwa.

Poleni sana Basata. Mmepuyanga na uamuzi wenu. 219 ni wimbo wenye sanaa nzuri. Uvumilivu unahitajika katika kusikiliza yanayochoma.

Ndimi Luqman MALOTO

Huo mwimbo nami nimeusikiliza na kugundua kuwa hauna kasoro yoyote na umejaa FACTS

Ugomjwa mkubwa unaokabili watendaji wa serikali hii ya awamu ya 5, ni kujiweka kwenye kichwa cha Bosi wao Magufuli, kuwa kwa kuwa Bosi wao hapendi kabisa kukosolewa, basi kila Mkuu wa idara ya serikali,including hao BASATA kutetea ugali wao wasitumbuliwe…

Refer tukio lililomkuta Nape wakati ule wa kuunda Tume ya kuchunguza tukio la “kipenzi” chake Bashite la tukio “real” la yeye Bashite la kuvamia studio za Clouds Media, tena akiwa na askari wenye silaha…

Nini kilmtokea Nape??

Aliishia kutumbuliwa!

Ndiyo kitu kinachowaogofya wakuu wengine katika kutekeleza majukumu yao ya kazi…

Kuwa mtu hivi sasa siyo kuwa anatekeleza majukumu yake kwa weledi Bali kutokana tu na kutaka kumfurahisha Bosi wake Jiwe!!

Kwani kitu gani alichoongea Sugu kwenye wimbo huo ambacho ni cha uongo?

Ameimba kuwa wanataka kumshoot kama walivyomfanyia Tundu Lissu…

Kwani mtamzania gani asiyejua hivi sasa kuwa “wao” ndiyo waliom-shoot Lissu?

Ameimba kwenye wimbo huo kuhusu kupigwa risasi kwa yule Mwanafunzi Akwilina…

Kwani mtanzania gani hajui hivi sasa kuwa Polisi ndiyo waliohusika katika mauaji ya msichana huyo ambaye wala hakuwa na hatia na ambaye alikuwa ndani ya gari?

Kwa mastajabu ya serikali hii, kesi hiyo imefutwa na DPP kwa madai kuwa wameshindwa kumbaini Muuaji!!!

Hivi uongo huo wa DPP ni mtanznia gani atakayemwamini??

Wakati sisi wenyewe tulimsikia kamanda wa Polisi wa kanda maalum ya Dar, akikiri mbele ya waandishi wa habari kuwa mmoja wa askari wake ndiye aliyehusika na maiaji ya mwanafunzi yule

Na Jeshi hilo lilikuwa likiwashikilia Polisi wake 6 kuhusiana na tukio hilo

Hii nchi kuendeshwa kwa matakwa ya mtu mmoja ndiko kunakoipeleka nchi hii shimoni

CCM WAMEUPIMA HUU WIMBO KWA RULA NA KUONA KUWA HAUKIDHI VIGEZO. MSIPENDE KUBISHANA NA CCM

Ngoma ni kali sana, halaf flow ya Sugu tangu enzi za Nipo mikononi mwa policcmm haichujagi

https://support.google.com/youtube/?p=report_playback

Wacha niisikie

Aisee! :oops::oops::oops:

Serikali haitaki kuambiwa ukweli ndio maana wakaleta sheria ya kuvidhibiti mitandao ya kijamii na vyombo vya habari.

Serikali haitaki kuambiwa ukweli ndio maana walimshoot T.L

Serikali haitaki kuambiwa ukweli ndio maana maagent wao kama BASATA wanafungia nyimbo zinazochana ukweli.

Hawataki kukosolewa ndio maana wamezuia mikutano ya kisiasa kwa wapinzani.

Hawataki wananchi tujue ukweli ndio maana wakazuia bunge kwenda live.

ngoma kali kinoma, kila kitu ameongea ukweli… JONGWE

Kujistukia Ndio shida

Hata Mandela alipotoka namba yake ya ufungwa iliendelea kutumika tena kwaajili ya kukusanya pesa za kusaidia jamii. Kwakuwa tupo Kenya mwenye nao aupakue

Kama wameweza kwenda bank alipokopea Sugu na kuwauliza bank toka lini wameanza kukopesha wapinzani, hawawezi shindwa kufungia nyimbo bila sababu…

Time will tell…

Cc: @Mahondaw

hii traki iko poa sana

Kama hii hapa chini?

Song la JonGwe ni hatari kwa afya ya sisiemu

#219