Jamani hata MO!!??

Kuna hizi habari kwamba Mfanyabiashara Mohamed Dewji ametekwa leo asubuhi maeneo ya Collosium Gym , Oysterbay alipokuwa ameenda kufanya mazoezi…

Mwenye habari kamili atujuze.

======

UPDATES:

Mfanyabiashara maarufu nchini, ambaye pia ni mwekezaji wa Klabu ya Simba, Mohammed Dewji (Mo Dewji), anadaiwa kutekwa na watu wasiojulikana waliokuwa na silaha za moto, saa 11 alfajiri wakati akiingia kufanya mazoezi katika gym ya Colosseum, Oysterbay jijini Dar leo Oktoba 11. Kamanda wa Polisi Kinondoni, Jumanne Muliro athibitisha.

RPC Lazaro Mambosasa amesema Polisi Dar inafuatilia madai ya kutekwa kwa mfanyabiashara huyo maarufu nchini

UPDATE 1:

Dereva wa Uber amesema aliona watu 4 wakishuka kwenye gari dogo, wakiwa wamejifunika usoni, wakapiga risasi moja juu na kumchukua Mohammed Dewji

UPDATE 2:

RPC Lazaro Mambosasa amesema waliomteka mfanyabiashara Mohamed Dewji (Mo) ni wazungu wawili. Aidha, amesema msako mkubwa unafanywa kwa raia wa kigeni wote waliopo nchini kufuatia kutekwa kwa Mo Dewji

UPDATE 3:

RPC Lazaro Mambosasa amesema watu watatu wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa mahojiano kuhusu kutekwa kwa mfanyabiashara Mo Dewji

UPDATE 4: 1100HRS
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda amekanusha taarifa za kupatikana kwa mfanyabishara Mohammed Dewji, na kwamba taarifa zilizosambaa kuwa amepatikana sio sahihi.

RC Makonda ametoa onyo kali kwa yeyote atakayeibuka na kuanza kusambaza taarifa za uongo kuhusiana na tukio hili au kuligeuza na kulifanya mtaji wa kisiasa.

Bashite hajui kuwa utekaji ni chanda na pete ya kisiasa. Tusubiri matokeo.

Dikteta na mwanaye bila shaka wanahusika ili wapate pesa ya kulipia makontena yao bandarini.

nimeisoma body language mambosasa na bashite inaeleza kila kitu. Trust me wamefika ukingoni

Ni imani yangu kubwa sana kuwa CCM itaaondoka madarakani kwa aibu na fedheha kubwa sana.

Mkuu BAK1 unauliziwa sana kipande ile kule, kumbe uko salama inatosha.

Shukrani kwa taarifa Mkuu.

http://www.thecitizen.co.tz/image/view/-/4802358/medRes/2138176/-/mg690j/-/Kinya12102018.jpg

The Guilty are always AFRAID

https://www.youtube.com/watch?v=ow9B3gKT1_I

Full upuuzi yaaaaaaani

Kwa akili yako fupi. Angekuwa katekwa babaako usingeandika huu upuuzi wako hapa.

Makonda mbona hili limekukereketa?