JAMIIFORUMS INATIA HURUMA.

Nianze kwa kuwapongeza Maxence Melo na team yake yote kwa kuweza kuirudisha hewani JF og kipenzi cha watanzania wengi watumiaji wa social media, hakika amefanya jambo zuri na kubwa zaidi.
Ila nimejaribu kuingia kama mgeni na kajaribu kupekua forum kadhaa kuangalia nini kinaendelea, tahamaki nimegundua JF imekuwa kama Nchi iliyohamwa, yaani Nchi ambayo wakazi wake ama walishakufa siku nyingi kwa homa ya kipindu pindu ama vita hivyo nyumba zao zimebaki kuwa magofu.
Sikuweza kulog in kwa acc yangu kwa kuhofia usalama wangu dhidi ya ‘malaika’.

Maswali mengi yakaibuka kichwani mwangu…
[ol]
[li]Je, Jf itarudi kuwa maarufu kama mwanzo?[/li][li]Je, Max anafanya nini kuwahakikishia watu usalama wao kama mwanzo?[/li][li]Je, mijadala moto moto inaendelea kama ilivyokuwa mwanzo bila kuathiriwa na ‘malaika?’[/li][li]…[/li][li]… Nk. Kwa hakika Jf inatia huruma mno.[/li][/ol]

Imerudi kama boshen tu, ila hapo tambua yafuatayo yanasikitisha option inayokuja utaingia kwa id yako ile ile ila itakuomba kwanza uingize email yako tena na namba yako ya simu hadi utumiwe. Veritification code ndio utafanikiwa kuanza kupost, id itakuwa fake ila email na namba yako ya sim watakuwa nayo, tofauti na wengi wanavyozan eti tutajisalili kwa majina halisi je nikiweka la mtu mwingine watantambuaje?

Hapo watabana tu kwenye namba zenu za simu mziweke kisha mtumiwe veritification code ndio uweze kutumia, ili wakikuhisi wakukamate kilainii… Wait and see jf sio salama tena

Hahaah ulishawah kuona mtu anarudi nyumbani kwake kwa kunyata? Ndio kinachotokea kwa JF members

Duu JF jamaniiiii.So sad.

Hahaha anasikilizia.

Swali namba mbili ni lamuhimu saana

Kwani we mwanzoni ulijisajili kwa njia gani?
Ukishaweka email yako si ndio ndio ina kila kitu pamoja na hiyo namba ya simu

Watu wengine bana full ujuaji. Email uliyoweka mwanzon ina kila kitu chako hadi IP address wanayo JF so wakiamua kukuuza dakika 0 tu ushapatikana.

Hata hapa KT hatupo salama

Huu ndio ukweli mtupu

Naked truth (ukweli ulio uchi)

Ukimya mwingi unakishindo…

Patamu, kwani kuna shida gani? mbona wadau huko fb wanatukana matusi ya nguoni na majina kamili na picha zao???

Mkuu kwa Utaratibu huu wa sasa naona lazima TCRA nao wawe na hizo taarifa zako we unafikiri uhuru utakuwepo tena

:D:D:D:D:D…

Kwa hiyo na wewe unataka kujilipua?..

Kama ni hivyo kwaheri JF

Naona ni kama kuna kujisajili upya au kujitambulisha info zako; maana uki - login huwezi post kitu chochote - kuna jambo, ile nyumba bado ya moto wacha tuendelee huku kwanza ugenini. au nyie wenangu vipi??

Kwa hili la kutoa taarifa zako wachangiaji JF watakuwa wachache mno. JF wameibana, unless iwe hosted kwengine, lakini je itajiendeshaje huko? Je anonymous members mtakubali kuichangia ijiendeshe??? Office, Mishahara ya MOD’s, Pango, Server Maintenance etc

Hapo ndo JF wanabana hawakubaliani na TCRA na hata wakikubaliana nao hawatakua na uhuru maana jamaa wataigeuza JF kama TBC1

[ATTACH]180249[/ATTACH]