Jinsi ya kupika vileja

Nadhan tunafaham vileja vikoje, ni jamii ya biscuits viko vya aina nyingi lakini leo ntaeleza namna ya kupika vileja navyojua mie

Mahitaji

Unga wa ngano kg 1
Mayai 4 hata 3 sio mbaya
Siagi nusu
Sukari itategemea unataka vya sjkari nyingi zaidi au kiasi
Baking powder

Namna ya kutayarisha

Chukua siagi na sukari mix kamavile wafanya kwenye keki changanya had uone sukari na siagi vimechanganyika kabisa

Weka baking powder kijiko kimoja cha chai usijaze sana

Changanya tena baking powder na mchanganyiko huo hapo juu

Vunjia mayai yako yite kwenye mkorogo wako then changanya had uone yai limejichanganya na siag na sukar yana kama vile kwenye keki

Mimina unga wako kidogo kidogo huku ukichanganya kwamkono kama vile unakanda unga

Hakikisha haviwi vigum sana wala lini sana viwe kati kwa kat

Tayarisha kibao chako cha chapat na mskumio na unga kidogo wa kushikia

NyunyiIa unga kwenye kibao chako wakat huo ule mchanganyiko wako umekata matonge tayar kwa kusukuma

Najua mtajiuliza why hapa vjnaoneaka kuna heart shape round shape hivo n vbat special kama huna tumia glass tu ya udongo ile

Hakikisha husukumi sana wala kuufanya mzito sana then zungushia glass kwenye unga wako uliosukuma kupata shape

Fanya hivo kwa matonge yaliyobakia

Chukua kiokeo chako hata sufuria pakaza mafuta panga vileja vyako

Vioke kwa mtoto mdogo mdogo had upate rang utakayo

Wabillah taufiq

@Madame S

[ATTACH=full]177922[/ATTACH]

Sawa

Kwa hiyo mimi Villager Elder ni jamii ya nini:p:p:p:p:p:p

Hahahhahawewe jamii ya doughnuts

:p:p:p:p:p:p:p:p:p

Yum yum
Nalog off

Hapo ni full utamu

;);):wink:

Upate na juice asee vinavyomumunyikia mdomon napenda sana

Kabisaaa

:cool::cool::cool::cool::cool:

Nn sasa

Ntajaribu kupika na mimi.

Ulete mrejesho

Usiogope madame