JINSI YA KUPIKA VITUMBUA
MAHITAJI
Mchele kilo 1
Nazi kubwa 2
Hiliki kiasi
Sukari robo kilo
Hamira kiasi kijiko kimoja nusu ( itategemea aina ya hamira)
Mafuta nusu lita
JINSI YA KUTAYARISHA NA KUPIKA
-
Uloweke mchele uliokwisha uchambua vizuri na kuupeta.
-
Utandaze sehemu safi ukauke, kisha usage upate unga mlaini
-
Kuna nazi uchuje tui zito
-
Saga hiliki, changanya na sukari
-
Changanya ule unga wa mchele, sukari, hiliki, tui la nazi na hamira. uvuruge uwe mwepesi kiasi cha kuweza kuchoteka kwa upawa.
-
Acha uumue kwa dakika 25 hadi 30 kutegeme na ubora wa hamira.
-
Weka kikaango cha kukaangia vitumbua jikoni, anza kukaanga vitumbua vyako kwa kueka mafuta kwanza yapate moto, kisha unachota kwa upawa unga na kueka kwenye vijungu vya kikaangio chetu.
-
Acha vichemke upande mmoja, kisha unageuza upande wa pili, vikishaiva vitoe weka kwenye chujio ili mafuta yajichuje.
-
Endelea kukaanga viliobakia mpaka unga uishe.
-
Ukivipata vya moto moto na chai pembeni vitakukosha sana
NB ; NAZI NI KWA AJILI YA KULA KiFAMILIA UKIPIKA KWA AJILI YA WATEJA UTAKULA HASARA . MASOMO YETU YOTE NI BURE KABISA
Follow
@JinsiYaKupika