Formulae no 3 (flat D)
na Emmanuel kasomi
Jinsi ya kutengeneza sabuni ya mche
Malighafi
-
Caustic soda vijiko 27 vya chakula
-
Maji chupa 239 soda
-
Mafuta lita 2 ( mafuta ya nazi,mawese,nyonyo au mbosa)
-
Sodium cilcate 1/2 kg
-
Rangi ya sabuni kijiko 1 cha chai
-
Industrial salt vijiko 3 vya chakula
-
Harufu kijiko 1 cha chai (perfume)
-
Hydrogen peroxide vijiko 4 vya chakula (kwa ajiri ya kuondoa rangi ya mafuta na kuongeza wingi wa sabuni.
Hatua za kufuata
-
loweka caustic kwenye maji kisha koroga kwa dk 15 na uache kwa kati ya siku 1 ama 20 hours.
-
siku ya kutengeneza sabuni injika mafuta jikoni na yakichemka tia hydrogen peroxide kidogokidogo huku
ukiyaangalia mafuta yako kwa kutumia karatasi nyeupe kama rangi imetoka yote. -
Baada ya hapo chukua maji ya caustiki soda,tia sodium,chumvi,kama unapenda rangi weka na
kama unapenda harufu weka huku ukikoroga kwa nguvu na kwa spidi hadi dk 15.
- Andaa ndoo ya plastiki na utie mafuta uliyoyaandaa na hakikisha yamepoa.anza kuyakoroga
kuelekea upande mmoja huku ukimimina ule mchanganyiko wako wa causiki kwenye mafuta kwa
mchuruziko kidogokidogo huku ukikoroga kwa nguvu zako zote hadi utapomaliza na baada ya dk
10 hadi 15 hivi mkorogo wako utakuwa tayari.
- Kamimine kwenye umbo na usubili sabuni
ikauke na baada ya dakika 45 sabuni yako itakuwa tayari kwa matumizi.