John John Mnyika mwakilishi kamili wa wananchi udumu kijana

Dakika tatu za MNYIKA Kimara, Technical Knockout (TKO)…

Leo nimejikuta nakumbuka pambano la ngumi uzito wa juu ambalo tulipewa hadithi nyingi na kulazwa alfajiri Kati ya ya Mike ‘iron’ Tyson na François Botha, pambano lilitangazwa ipasavyo!

January 16, 1999 Tyson alimchapa Botha (white Buffalo) kwa Knockout. Raundi ya Tano. Hapo Tyson akwa na rekodi dhaifu mbele ya Botha.

Mapambano ya Tyson 45(3) Botha 39(1) na wakati huo Tyson akiwa na mikanda ya WBC, WBA na IBF nafasi ya 10 kwenye ubora. Botha nafasi ya pili akiwa na mkanda wa IBF

TYSON akitoka kucheza na Evander Hollyfield June 27, 1997 pambano ambalo Tyson aliondolewa ulingoni baada ya kumuuma sikio Evander.

TYSON akapigwa faini ya $3M na kamisheni ya michezo ya Nevada ikamnyang’anya leseni yake. Baada ya kukosekana kwa miezi 15,anarejea na kupewa François Botha.

Kauli ya Tyson ikawaogopesha wengi, alisema “ninakwenda kupambana nae usoni, natarajia atakwenda Chini wa baridi. Natarajia atakuwa Marehemu, nitamuua”

Ajabu katika pambano hilo, raundi ya kwanza tu, mwamuzi Richard Steele alipowaachanisha mabondia waelekee kwenye kona zao, wakaendelea kurushiana ngumi, hadi walinzi wa MGM GRAND kuingia ulingoni, kuachanisha.

Pambano likaendelea, baada ya onyo, raundi ya pili. Botha akashinda raundi ya 3 na 4 na raundi ya tano akiendelea vizuri, sekunde 12 zimesalia, Akapigwa ngumi, iliyompeleka Chini.

Wakati TYSON akitoka kufungiwa kwa miezi 15 bila kupigana ulingoni, John Mnyika anatokea Mbeya kwenye ziara za CHADEMA, akiwa na kumbukumbu ya kuzuiwa kufanya siasa hadi 2020, anapata jukwaa mbele ya ALIYEZUIWA!

alichofanywa François “white Buffalo” Botha kutoka Pretoria, RSA, raundi ya 5 na Mike ‘Iron’ Tyson pale MGM GRAND ndio kitu MNYIKA amekifanya kwa ustadi kabisa kwa dakika tatu, Saranga, Kibamba! KNOCKOUT! MNYIKA akichapa “technical”

Mbunge wa Kibamba katumia dakika tatu kueleza mengi ambayo yangeweza kubebwa katika hotuba ya dakika zaidi ya 60, kaivuruga kabisa hata hotuba ya Magufuli.

Baada ya John Mnyika, wamefuata wabunge wa CCM na Mkuu wa mkoa wa DSM, wakapwaya ipasavyo mbele ya ujazo wa dakika tatu tu za MNYIKA jukwaani.

Wakati Makonda anauliza “KWANINI wapinzani wanamkosoa Rais?” wakati Makonda anashangaa uwepo wa wabunge wa CHADEMA katika eneo hilo, ni wakati amepigwa “TKO” maridhawa. Kabisa!

Ukimsikiliza John Mnyika, ukarejea kuwasikiliza wazungumzaji wengine wa upande wa serikali na viongozi wa CCM, unagundua, hawa walipigwa TKO na Mnyika raundi ya kwanza kabisa…

Wakati Mnyika akiongelea uchumi wa watu kuporomoka, wananchi kulipwa fidia, hali ya. Kidemokrasia kusiginwa misingi yake, watu wa CCM na Makonda wanamwaga pongezi kwa Rais!

Nimesikiliza majibu ya Magufuli kwenye hoja za Mnyika, ameonekana wazi ‘kupaniki’ na kushindwa kutambua msingi wa maswali ya Mnyika! Mnyika amekuwa ‘TYSON’

kwa namna yoyote ile, Rais Magufuli, na Wapambe wake wote ambao wameongea katika shughuli hii, tunawaweka katika kona ya François Botha. Wamepigwa kabla ya raundi ya Tano kumalizika

Mnyika, katumia dakika 3 na sekunde 20 kumaliza mchezo wake, kata ya saranga, mtaa wa Stop over jimbo la Kibamba, akiwaacha kona ya BOTHA wakipigwa na butwaa. MNYIKA, amegusa nyasi zote za uwanjani.

Kama ambavyo Botha alikuwa akilalamika kwa mwamuzi Tyson kumchezea ‘faulo’ Mnyika kampongeza Magufuli kujenga Barabara Kibamba, lakini akamuachia maumivu ya kilio cha wananchi kukosa fedha na vyuma kukaza!

Mnyika akimkumbusha alivyoomba kuombewa kule Arumeru ili aachane na KIBURI, hivyo awasikilize wananchi wa Ubungo na Kibamba na vilio vyao, awalipe fidia za ‘BOMOA-BOMOA’ huu ni mtego dhahiri. Akili kubwa.

Wakati Mnyika akisema kuhusu Maendeleo na Demokrasia kuwa pacha, hivyo Rais azungumzie hali ya kisiasa, Magufuli anasema, ‘kusengelikuwa na demokrasia Mnyika asingepewa nafasi ya kuongea, aliyoongea’

Wakati Mnyika akisema kuhusu wananchi wa Ubungo na Kibamba waliopisha ujenzi wa Barabara kulipwa FIDIA, Rais anasema "hakuna FIDIA ambayo italipwa kwa sababu serikali ilishinda kesi mahakamani’

Wakati Mnyika akimkumbusha Magufuli kuhusu kuondoa vikwazo ya kidemokrasia ili nchi isonge. Kasi kimaendeleo, Magufuli anasema “siasa za kubembelezana zimefika mwisho” hapa nafikiri Mnyika ameshinda ‘raundi hii’ bila kipingamizi!

Mnyika ametumia falsafa ya “ukikutana na Macho ya mfalme, eleza anayopenda kusikia, ukichomeka na shida zako na mfalme atakuona u-mtiifu sana kwake” na ndio kitu kimefanyika.

Wakati Magufuli anasema Mnyika anapaswa kuipongeza CCM kwa kumletea Maji kwenye jimbo lake, Magufuli anakwenda mbele na kujipa jibu, “Mnyika aliyapigania san maji” kumbe ni wajibu wake!

Baada ya Mnyika kumaliza ya kwake, kwa dakika Tarun pekee, Magufuli ametumia zaidi ya dakika 30 kueleza yatokanayo na dakika tatu za Mnyika. Tyson, Iron, Man of the Day!

Ukimsikiliza vyema Magufuli, katika maneno yake, ni kama John Mnyika aliharibu ramani nzima ya alichopanga kusema, ikabidi acheze kwenye ramani ya Mnyika. Mnyika ameshinda raundi zote kutoka Kibamba!

Hivyo, Mnyika ametupunguzia darasa kubwa ambalo tunapaswa kuwapa wabunge wetu. Wakiwa mbele ya Mfalme. Wanapaswa kuwa kam Tyson na kumgaragaza Botha mapema na kumuachia maumivu, atajikanda mwenyewe!

“MSEMINARI” John Mnyika, Hongera, haujasema kwa ajili ya CHADEMA pekee, umesema kwa ajili ya wengi, ukweli wa hadharani kwamba “vyuma vimekaza” sio kwa MAFISADI TU, hata kwa wananchi wa kawaida…

#MMM, Martin Maranja Masese

[emoji120][emoji120][emoji120][emoji120][emoji120][emoji120][emoji120][emoji120][emoji106][emoji109]

Kwa sababu hizo ndiyo maana hapendi kuwaalika wapinzani haswa wale vichwa…

Anaalikaga wale wapinzani ambao watasimama mbele yake na kuhamia kwenye chama chake…

Cc: @Mahondaw