Kama una stress pitia hapa, usiache na wewe kutupia maneno yako!!!

Huku tukiendelea kupunga upepo huku kwa majirani zetu, tuendelee kupata burudani na kutoa stress kwa huu uzi wetu pendwa…

Leo kidogo nipigwe na MWANAMKE baada ya LIFTI kusimama…wakati tupo kwenye lift Nilikua nayaangalia MAZIWA yake akasema "Bonyeza Moja"mi si nikalibonyeza?
Yaani had sasa
bado najiuliza nilipokosea.

Hivi Utajisikieje Utakaposikia Rafiki Yako wa Karibu Hajaja Kwenye Mazishi Yako ???!
Nadhani Mimi Sitamwongelesha Tena !!!
I think nakaribia kupona

[COLOR=rgb(209, 72, 65)]Nimenunua chips ili nile kwa bahat mbaya mtoto wa mama mwingine amekaa next to me akaanza kuzililia.
Imebidi nivae earphones. Napenda watoto, ila utoto ndio sipendi…

Jana nimepita njia ya mkato makaburini warembo wawili wakawa wananikimbilia wanatetemeka Eti tunaogopa kupita peke yetu na mm Nikawajibu hata mm nilivyokuwa hai nilikuwa naogopa sana . Wakazimia
Sipendagi kufatwa fatwa m

Siyo shida mtu mwenye sura mbaya akiwa rafiki yako, shida inakuja pale anapoanza kukuita “pacha”.

Unasema hupendi ujinga na unatumia tecno!:cool::cool::cool:

Ahahaha!! Nimecheka sana.

:p:p:p:p:p:p:p:p:p:p:p:p:p

Mwendo ni ule ule

Yes, tunalisongesha mwendo mdundo…

Kuna wanawake kama mashetani tu! yaani, tumekuta msibani tukabadilishana namba akani save eti mzikaji…!!

Mwendo mdundo

hahahaha duh

Inamsaidia kukumbuka kwa urahisi…

Picha mbaya ya roadside kiosk ni kupata mende kwa chakula na ya watu wenye tambia zao ni kuchanganya avocado na mandondo.

usipende kubonyeza mkuuuuuuu

usipende kubonyeza mkuuuuuuu

Duuuuuuuu

Unawatoa out madada, then bili inakuja around 6M, unaamua kuondoka kimya kimya watajijua wenyew…
Kwa mfano huyu Legend hapa anahitaji tuzo kwa kweli R.37k, halafu kawachinjia baharini mtu kapotea… hahahhahaha

Una VITZ unapeleka car wash ya nini? Si uchanganye na vyombo uoshee tu nyumbani…

Demu mweusi hatongozwi gizani wewe…
Utaachwa unaongea mwenyewe kumbe yeye keshaondoka oooooohh!

Kweli stress ltoke kkkkkkkk
Nalog off

[ATTACH=full]176647[/ATTACH]

Customer Care ya Wadada wa Saluni za kiume iko juu sana…yaani anaweza hata akakuchanganyia upupu kwenye Scrub na muwasho ukausikia ukiwa nyumbani!.. hapa unaweza hata kubandikwa lami ya strabag kwenye kipara na bado ukahisi ni easy wave!.

Kuna ile kitu inaitwa Massage ya kichwa,…aisee hapa hata uwe Jenerali wa jeshi lazima utakuwa mpole kama anaungama!,…yaani unakuta mtu kasinzia anakandwa utosi huku analamba midomo kwa raha kana kwamba kapata Scholarship ya kusomea Gesi huko Freiburg Ujerumani!.

Unaambiwa “Kaka tukupake na dawa ya mba?..NDIYO NIPAKE…je Scrub ya Maboga ?”…unajibu tena NDIYO"…hujakaa vizuri unasikia “tukuwekee Tango kwenye Kidevu?”…Unajibu NDIYO!'…halafu unasikia tena "Tukupake Limao kwenye Upara?..hapa napo jibu ni NDIYO kana kwamba unapokea ufunuo!

Mwisho wa siku unaletewa Bili laki moja na thelathini na tatu-133,000/-!..na hapo sasa ndipo unapomuona Bwana Israel mtoa roho ameketi jirani yako nae ananyolewa kiduku…!