Kama Wanafunzi wa siku hizi wa Udaktari ndiyo wako hivi acheni tu watutibu ndivyo sivyo na Watuue!

[FONT=courier new]Hivi inawezekana vipi kweli Wanafunzi wa Fani ambayo Mimi GENTAMYCINE ndiyo naamini ni ’ Nyeti ’ kutokana na umuhimu wake kwa Binadamu muda wote unawakuta wako tu Baa ’ wanagambeka ’ na wengine kutwa tunakutana nao katika ’ Makorido ’ ya Gesti kama siyo Loji wakitoka ’ Kubanduliwa ’ na yote haya wakiwa wanayafanya muda ule ule wa Vipindi vyao Madarasani.

Angalau sasa nimeshajua kwanini huwa tunaachiwa Mikasi matumboni na matakoni, oparesheni za Kichwa tunafanyiwa katika Ugoko na unaumwa Malaria unapewa dawa za Kuongeza nguvu za Kiume yaani ni vululu vululu tu.

Kuna Mtu mmoja aliniambia kwamba ni kheri niende nikatibiwe hata kwa gharama kubwa Agha Khan Hospital kuliko katika Hospitali zingine zote ambazo sijazitaja kwani 98% ya Madaktari ambao wako huko hawana ’ Uweledi ’ na wengi wao wamefaulu na kuwa hapo kwa ’ ujanja ujanja ’ huku wengine ’ wakihonga ’ lakini kiuhalisia uwezo wao wa Kutibu ni mdogo sana.

Sasa yote tisa kumi kuna Hospitali moja hivi nipo nayo jirani kabisa ila siitaji kwakuwa Wao wana msemo wao mmoja wa ’ Kibabe ’ hivi usemao '[COLOR=rgb(184, 49, 47)] Sadism is inevitable when the situation is alarming ’ na huwa wanaumaanisha 'Kivitendo ’ hasa. Na bahati nzuri aliyeniambia ni mwenzao na nakumbuka maneno aliyoniambia namnukuu…" GENTAMYCINE kama siku ikitokea Shemeji yangu ( anamaanisha Mke wangu ) akiwa amebeba Mimba yangu halafu anataka Kujifungua usipoteze muda wako kumpeleka katika Hospitali yetu na ikitokea ukampeleka Kujifungulia hapa jua mambo mawili ama umpoteze Shemela au Mtoto wako au wote wawili…"

Tafadhalini sana enyi Wakufunzi / Wahadhiri wa hivi Vyuo vya Udaktari hapa nchini Tanzania jitahidi mtoe Elimu bora kweli ya Tiba kwa Wanafunzi wenu ili basi Tanzania ile ambayo ilikuwa inasifika kwa kuwa na Madaktari ’ mahiri ’ kabisa irudi tena kwani siyo Siri hizi ’ Products ’ zenu za sasa ni za ’ hovyo hovyo ’ mno na ’ wanaharibu ’ sana huko Wodini kunako Mahospitalini.

Wewe Mtu anasomea Udaktari lakini asubuhi katika Kijiwe cha Kahawa namkuta, nikienda Kijiwe cha Kusoma Magazeti namkuta, nikienda Gesti / Loji ’ Kubandua ’ nakutana nae, jioni nikienda Kuangalia Ndondo Cup yupo na usiku nikienda ’ Vibanda Umiza ’ kuangalia Mpira wa Kombe la Dunia tena nakutana nae na hapo ni siku ya Masomo halafu unanimbia eti huyu siku ikitokea ninaumwa nimpelekee kabisa huu mwili wangu akautibu. Nina uwazimu au?

Badilikeni!

Nawasilisha.[/FONT]

Kuna umuhimu wa kuwa na ukaribu na @Mshana Jr

duu.we acha tuu.

Hatari sana