Ndugai amedai kuwa wabunge wakiikataa bajeti, rais atalivunja bunge na kwamba eti kuna baadhi ya wabunge wakirudi kwenye uchaguzi majimboni mwao hawatarudishwa bungeni.
my take:
nchi yetu haijawahi kuwa na spika kilaza kama huyu. ni aibu kubwa kwa spika kukosa uimara hivi.
anyways, nadhani pia anajihofia mwenyewe kwani ilibidi amtandike mtu bakora ili jina lake lipitishwe na chama chake dhalimu!
Kama wawakilishi wetu wameiona bajeti pendekezwa haina tija kwa mwananchi ni vyema sana kwa waziri wa fedha kufanya marekebisho hasa kwenye maeneo ambayo inaonekana yana matatizo ili bajeti iwe halisia na ya kutekelezeka kuweka hofu kuwa isipopita basi Rais atavunja bunge basi tuipitishe hivyo hivyo ni kutowatendea haki wananchi maana wao ndio watakaoingia na bajeti hii inayoonekana haifai.
Spika anapaswa kusimamia haki ili bajeti iwe ya manufaa kwa nchi ili tusonge mbele tusiwe na bora bajeti bali bajeti bora
ndungai ni mpumbavu sana, kwanini anaitetea serikali??? kama anaogopa bunge kuvunjwa sasa kuna haja gani ya uwepo wa bunge kama kazi ya bunge ni kupitisha uharo wowote unaoletwa na Magufuri???
Miaka yote wabunge wa ccm huwa wanapitisha kwa kutishiwa kwamba bunge litavunjwa. Tofauti ya zamani na sasa ni kwamba vitisho hivi vinafanyika waziwazi. Ni kwanini wabunge wanaweza kutishiwa na wakatii hata jambo lisilo na tija? Ni kwa sababu wanapata malipo makubwa kinyume na uhalisia wa uchumi wa nchi.
Karibia 90% ya wabunge hawana uwezo wa kupata hela za kiwango cha mshahara au mikopo waipatayo kupitia ubunge. Na serekali kwa kuwa ina watu wa hivyohivyo wenye umasikini wanajua huo udhaifu. Hivyo wanafahamu fika wakitishia kuvunja bunge ni lazima watatii tu. Sioni mbunge anayeweza kulipa mkopo wa milioni 200 nje ya ubunge.
Hakuna umuhim wa kuwa na bunge basi,inaonyesha kabisa bunge linaendeshwa toka ikulu.Magufuli and his cronies don’t give a fuck about bunge or anybody’s else.
hahahahaha hii ndio sababu hamtogusa ikulu kwakuwa mnapenda kupenda kusikia yanayo wafurahisha tuuu…huyo amewambia wana CCM wenzie…hahahaha leo ndungai amekuwa mbaya?