Naija Yaipiku India kwa Kuwa nchi yenye masikini wengi duniani...

Licha ya kuwa mzalishaji kubwa wa mafuta, bilionea mkubwa afrika na duniani Dangote anatoka huko.
Licha ya kumiliki forum kubwa afrika nzima, yenye member zaidi ya millioni ambamo kuna mawazo malaki ya kufanikiwa.
Ni watu wajanjawajanja sana na wako aggressive na mafanikio hata huku bongo ukiwakuta hawana masihara na mambo yao.
Ni watu ambao wamejanjaruka (wanaexposure) na mambo ya ulaya siku nyingi.
Ni watu wenye Rais asiyependa masihara na mali za taifa, na anayajua matatizo yao maana amekuwa rais mara mbili.

CHA AJABU.
Watu Takribani milioni 87 ni masikini wa kutupwa na kuifanya nchi hiyo kuongoza kwa kuwa na wanadamu masikini wengi wakiipiku india ambayo
pamoja na ujuaji na ujanja wao wote wa kibiashara na maendeleo zaidi ya watu Millioni 73 ni masikini wa kutupwa.

source:Africaweekly.
Je, Jitihada zetu hapa Bongo zinatupeleka mbele au tunarudi nyuma kuwa makao makuu ya umasikini duniani katikati ya utajiri wa asili.
Kilichoniogopesha Taifa ilnaweza kuwa masikini mno katikati ya Utajiri. Kuwa na makorokoro mengi ya maana sio kigezo cha utajiri.

Duh!.. :oops::oops::oops:

Kweli GDP norminal na GDP norminal per capita haiakisi uhalisia wa maisha ya wanadamu ktk nchi husika.

Iyo Forum Ya Dangote Inaitwaje

Duh balaaa hilo linainyemelea Bongo

sio ya dangote ni ya wanaija wenyewe.
inawatu zaidi ya millioni wakati hii kenyatalk naona hata 600 hawafiki na jf tulikuwa kama laki nne.
kuna majukwaa kule watu wanapeana ujuzi utadhani analipwa hatua kwa hatua.
forex ambayo huku tuliishadidia utadhani ni kitu kipya huko ilishajadiliwa miaka mingi sana na nasikia imepigwa na ban kujadiliwa ila sina hakika.
kwa ufupi wale wako mbele yetu kwa kuwa na exposure ya maendeleo na rasilipesa nyingi kuliko sisi lkn idadi hiyo ya masikini wa kitupwa inatisha.
bado Nollywood ni ya pili duniani nyuma ya bollywood kwa kutengeneza movie nyingi na wanaingiza matrillioni.

najifunza tu mkuu, unawezakuwa maskinitajiri.
forum hiyo ni nairaland.com

pia kumbuka ukiondoa china nchi zenye watu weng zaid dunian n india halaf ije hio nigeria, population mara nyingne n tatzo sana katika kutengeneza uchumi, japo huwez jitetea sana kwa hilo mana china wameshka karbun robo ya watu dunian ila ipo juu. Hizi statistics zao wangekua fair sana kama wangelinganisha nch zenye angalau population zinazokaribiana kama si sawa, hapo ndo utamjua zwazwa, ukiangalia hio idadi yao ya watu maskin n karbuni mara mbili ya watu wote Tz. Rwanda ina watu takriban M7, hv unatarajia idadi ya maskin rwanda iwe kubwa kulingana na tz yenye watu zaid ya M50? Je kwa kigezo hcho utasema rwanda au somalia imeendelea zaid ya Tz?

Nigeria ina kama watu 185 mln wakati India ina watu kama 1.2bln. kwahiyo watu 87 maskini ni karibu Nusu ya wananchi wa Nigeria wakati India watu 73ml ni tone tu kwa wahindi wote.

ila Waafrika tusipiwekeza kwenye kilimo cha kisasa na elimu tutapata sana shida huko mbele. ipo siku tutakulana.

TUTAPATA TABU SANA

Inasikitisha sana…

Cc: @Mahondaw

Nigeria inashika nafasi ya 7 ikiwa na watu takribani milioni 193, na inakadiliwa idadi kuongezeka mpaka m300 itakapofikia 2050

vipi tizii???