Hi,
Kwanza niwape pole wanawake ambao wamezaa watoto wao na wanawalea wenyewe.
Pili niwatie moyo kuwa wanaweza hivyo wajitume ili watoto wao wafikie malengo.
Tatu ningependa kujua changamoto wanayokutana nao wanawake hawa hasa katika malezi ya watoto.
Nne changamoto wanazozipata wanapoanza mahusiano mengine ilihali wana watoto.
Tano wanaume wanaowaoa wanawachukuliaje watoto wanaowakuta nao.
Tujuzane…
Mimi nadhani changamoto yao kubwa ile sisi wanaume kudhani kwamba bado watakua wanaendeleza mapenzi na wenza wao waliyowazalisha…
Mara nyingine inaweza kua kweli au isiwe kweli…
Cc: @Mahondaw
Ukizaa kwa mapenzi yako mwenyewe ni njema ila kama ulizaa kwa bahati mbaya basi ni shida …maana bado familia zetu nyingi zinamtazama vibaya sana kijana ambaye hajazaa afu anaenda kuoa mwanamke aliyezaa.
Doncute:
Hapana…muke ya mtu
sasa kwanini unataka kuyajua ya upande wa pili…
Mara nyingi ni ukweli 87%
Kweli ni mara nyingi zaidi,hasa kama mazingira ya kuachana hayakuwa ya ugomvi…
Wanasemaga wazazi huwa hawaachani hii kweli bwana sio utani.
Hii mada imeanza tena huku ugenini!!
Kyaka
June 18, 2018, 5:34am
17
Habari za ugenini wa TZ wenzangu?
wanawachukulia poa tu
shida ipo kwenu umkute mwanaume na watoto huwa mna roho mbaya hakuna mfano
Yani wanawake wengine wanaroho za chuma…watoto wa mwanaume watanyanyaswa mno…