Tuliopitia chereko chereko tukumbushane ile siku.

Ninakumbuka dada na shangazu walinisaidia kupanga sanduku usiku wa kuamkia Jumamosi. Huku wakiniusia kuwa ndiyo nimekuwa mke wa mtu. Yale mambo ya kukaa kwenye makochi nikisoma novel itabidi niyafanye baada ya kumpikia mheshimiwa.

Asubuhi mrembaji alikuja, hata sikuwa na njaa japo nililazimishwa sana kula. Nilikula mishikaki tu baada ya kuagiza kiepe kilichonishinda.

Baada ya kupambwa tulianza safari, Sandusky langu likiwa nyuma ya gari huku nikiimbiwa snameremeta. Yakwangu ilikuja ni kuwa 30+.

Nakumbuka tu nilivyofundwa…kuwa mvumilivu kwa mume wangu…

Siku ya sherehe…ule wimbo…wa kwetu…mwai wetu eo hio tuenda tumuvone…luvoo la mwana luwaja aee luwaja…luwaja kangi ugure mtwii…

Natamani irudie tena

Naona akina mama mnakumbuka jinsi mlivyoasiwa na ndugu zenu huku mkuagwa. Hongereni saana.

sijui lini nitakubali kuoa

halafu muoaji huwa anachukulia simple tu ila balaa lipo upande wa pili

Utaoa tu wakati wako ukifika

Usiache kunilika rafiki muda ukifika

Kumbe Tangaline! Mapenzi yalikoanzia…

mkuu wakati kama ushapita,nakaribia 40
kinachonipa jeuri ni kwamba nina mtoto

mkuu nakaribia 40
nafikiri kwa vile nina mtoto ndo maana
stress za kuulizana uko wapi kila mara sijui kama nitaziweza

ilikuwaje usiku huo? wiki hiyo? i hope mlikuwa mkikesha

Send off ilikuwa tayari Ila usiku huu kulikuwa na sherehe nyumbani, vijana na DJ wao, mdumange na shime kule na wazee wakijinywea taratibu

kama mdumange ulikuwepo, uko vizuri

Mara nyingi akinamama huwa wanapata MP sababu kuu ikiwa ni kupania harusi. Kwangu ni siku sipendi kuikumbuka maana nilichukia sana hata huwa sitaki kuona picha za harusi.

pole mkuu…mi pia siipendi kwa sababu moja tuu, nilishindwa kula vyombo ukweni

Baada ya sherehe si unaondoka na mke wako kuelekea hotelini?

In fact unavyohaidiwa na mchumba akiwa mke hola.

Haha kwanini hutaki kuoa?

wanawake wote nahisi ni walewale
niliwahi kuishi na mdada unofficially niliuona mziki wake

Wako wengine tofauti bwana