Ugenini

Habari

kuna thead moja wakati ule wa uhai wa jf, iliyokua inaelezea jamaa alivyotembelea drc congo, na namna tunavyochukuliwa wabongo huko congo. Ktk maelezo yake alisema wacongo ni watu poa na wanatupenda na kututhamini sana wa tz kuliko nchi nyengine. Katika comment za “villager” wengi walisurpot tathimini yake na kuongeza nchi zengine zinazotuthamini na kutukubali wabongo, wakiitaja kenya. Yani mjadala ulikua nani namba moja kati ya mkenya na mcongomani kwa kutujali pindi tunapokutana viwanja nje na aridhi ya nyumbani. Sasa ninachoshangaa, au hoja yangu, tangia tumekuja huku kt ugenini, comment za wakenya ni tofauti na tulivyoaminishwa kwamba wakenya ni ndugu zetu na hawana chuki au kuonyesha chuki kabisa baina yetu. Mbona comment za wakenya wanaonekana kuchukia wa tz sana.

Wapo wazuri na wapo wahovyo…

Wasikuumize kichwa hawa mkuu wachukulie kama walivyo maisha yaendelee

Usiwachukulie serious sana kwa humu, nenda nao vile wanataka.

Ukiwazoea wala hawakupi shida.

take easy! saivwashaanza kulegeza si ka mwanzo tulivoanza kuingia hum

Post zaidi ya elfu ishirini na tatu jamiiforum KT. Watanzania wameamua kufanya kweli!

Theads kama 652 now

Wanatucheka tunavyowrite comment, tunawrite like insha.

Mbona

Mbona sija muona mkenya hata mmoja ameongea hovyo juu ya mtanzania?wa tz msiwe na hio roho bana.
Kama una sema kuna chuki dhidi ya wa tz ni vyema kusema mkenya ali fanya hiki ama lile kudhalilisha mtz.
Bila evidence ni projo na maneno ya uchochezi tu kutafuta likes tu.

Wanakubali kiaina

Establishment inajuta, mashambulizi air to ground missiles ndio yanaongezeka kila kukicha.