Ujumbe kutoka kwa Henry Kileo mume wa Joyce Kiria

Ameandika Kamanda Henry Kileo mume wa Joyce Kiria katika ukurasa wake wa Facebook.

Hakuna chochote katika maisha cha kupigania!

Nguo zako zile bora kabisa kuna mtu kwake ni matambara tu.

Akiba yako kwenye akaunti ya Benki ni sawa na mchango wa mtu katika sherehe tu.

Boyfriend au Girlfriend wako au mchumba ni Ex wa mtu!

Hivyo ni nini hasa cha kujivunia?

Maisha ni mafupi sana na madogo mno kujisikia kuwa mkubwa ama bora kuliko mtu wengine.

“Tupo sote uchi hadi kufa” aliwahi kusema Steve Jobs. Gwiji muanzilishi wa iPhone(ambaye kwa sasa kifo kimemchukua kwa maradhi ya Cancer)

“Hakuna kitu kinachoweza kutuokoa sote Kukabiliwa na kifo”.

Naumia kuona watu ambao hujivunia utajiri, uzuri, akili, kiwango cha elimu, umaarufu na vitu vingine vya tamaa za kimwili, kwani hakuna jambo umefanya la mafanikio katika maisha yako ambamo halijafanywa na mtu mwingine ama kupitia

Cheo unachomiliki ofisini leo kilikuwa kinamilikiwa na mtu mwingine kabla na kitatwaliwa na mtu mwingine baadaye, wala hujui mtu huyo anaweza kuwa nani

Kuna jambo moja tu la thamani la kujivunia ambalo ni “MAISHA ndani ya Mwenyezi MUNGU Muumba”.

HIVYO ni vema kuwa mwema kwa Jamaa zako na daima tengeneza Marafiki!

Daima kumbuka kwamba watu unaowakanyaga wakati ukiwa njiani kukwea ngazi kwenda juu huenda wakawa ni walewale utakaowakuta kwenye safari yako ya kuteremka ngazi

Hivyo jitahidi usiwe tatizo kwa watu wengine au kufanya maisha magumu kwa mwingine kwa kutumia nafasi yako, kwa sababu kwa wewe kufanya hivyo ipo siku watu hao hao wanaweza kuwa kikwazo kwako siku moja mbeleni.

Kumbuka,hata jani la mgomba wa ndizi kuna siku litanyauka na kuwa majani makavu yasiyo na ukijani tena!

Tafadhali usiwe na Ubinafsi, Wajulishe marafiki wengine kuwa sote tupo njia moja.

Kama siku moja utajisikia kulia, niite. Sina ahadi ya kukufanya ucheke lakini naweza kulia na wewe.

Kama siku moja unataka kukimbia kwenda mbali usiogope simu yangu.Niite nami nakuahidi kukimbia bega kwa bega na wewe!

Lakini, kama siku moja utapiga simu yangu na haina majibu basi njoo kwangu, Huenda nakuhitaji wewe.

Siku moja, mmoja wetu hatutakuwa naye hapa tena na utasikitika juu yake lakini ukiwa umechelewa kwani hutokuwa na nafasi hiyo tena!
Machozi yanaweza kukutoka!,lakini itakuwa umechelewa. Kwa hiyo, mkumbushe na kumwambia kila mtu kama vile ambavyo mimi nimefanya!

Very true

Ni ujumbe mzuri sana kwa Jiwe na mwanaye, ambao wanajiona “wamefika” na hata msamiati wa kifo hawajui maana yake!

Eeee egheeeeeeee…!!! naona hapa kila Mtu na Kilio chake…!!! Watakuja wengine wa Maswala ya Mapenzi, Familia, kudhulumiana na mengine…!!!

Tatizo binadamu ni wabishi sana…

Cc: @Mahondaw