Vodacom wanidhulumu pesa ndani ya MPESA

Ijumaa iliyopita nilisafiri kwenda Dar kutoka Nairobi. Kufika Dar nikanunua na kusajili line ya Voda na kutuma pesa kutoka kwa line ya Safaricom kwenda ya Voda na pesa zikafika. Nilitoa nusu yazile fedha na zingine nikaziwacha kwenye line. Hio ni Jumamosi mwendo wa saa kumi na moja jioni. Kufikia saa mbili usiku, Voda wakanitumia message kwamba line yangu haiko registered na MPESA. Fikia sasa bado sielewi kwa nini ilhali nikiwapigia simu wananiita kwa jina langu na line ilikua na pesa ndani.
Nimepigia Voda customer care lakini hawajanisaidia hadi wa leo. Inamaana hela zangu zimekunywa maji hivyo?

Mkuu nenda kwenye moja ya ofisi zao upate majibu ya kueleweka kwa sababu online customer care ni maigizo na maumivu.

Mitandao hii kwetu bado, watu siyo waaminifu, hivyo wizi ni mwingi. haya yanafaa ulaya tu na marekani. I will do the minimum with these mitandao, mitandao yoyote! Simu ndio usiseme, do the minimum! Mfano kama nasafiri, natoa hela kabisa one or two days before, usitegemee kuwa eti nitatoa kesho asubuhi wakati napanda Bus kwa mfano, UTAKWAMA! You go there and the blood hopeless thing is out of order! You get stuck!

Nenda kwenye branch yao yeyote, na usije ukawachekea. Komaa hasa hadi kieleweke.

Mitandao yetu si aminifu kabisaaa

nenda vodashop watakusaidia

Pole sana…

Wanazingua sana…

Cc: @Mahondaw