Wachaga na mambo yao.

WACHAGA wako radhi waache wake zao moshi mwaka mzima ili wakasake pesa DSM. Moshi wanarudi Xmass. Hivyo usimulize kama watoto hawafanana na baba au jirani na kwani kitanda hakizai haramu!

UTANI WA WACHAGGA.!!
Wachaga wamegawanyika kama ifuatavyo, sio wote wajanja. Kuna:-

  1. WAROMBO; Hawa wajanja sana kibiashara/wezi pia. wanapenda dili za magendo. Ni walevi sana hupeleka wake zao vijijini wakileta kiburi mjini. Wanaume wa Rombo wanachunwa sana na wanawake wa Marangu na wanawaita “vishohia”. Wanawake wa Rombo ni mama Huruma, wanaachia tu… Ukioa Mrombo ujue umeolea kijiji.

  2. WAMARANGU; Ni wazuri sana wa sura na umbo, wanavutia. Lakini wanawachuna sana Warombo. Wanawake wa Marangu wana dharau sana na wanaume ni waoga kuliko wanawake. Mwanaume wa Marangu kupigwa na mkewe si jambo la ajabu.

  3. WAKIBOSHO; wanafanana na Warombo lakini ni wavumilivu zaidi. Biashara kubwa wanayofanya ni ya kuchinja… wengi wanamiliki mabucha. Wana hasira sana na ni wakatili… Akikuchoma kisu, siku ya mazishi anakuja kudai kisu chake.

  4. WAMACHAME; hawa ni wezi sana, ukifanya nae dili umeliwa. Ni wasiri sana lakini wako makini mno hasa kwenye pesa. Wakiwa na hasira hawaoneshi waziwazi, so Mmachame anaweza kukuua huku akitabasamu. Sio waaminifu sana lakini wanaenda kanisani mara nyingi zaidi kuliko Wachaga wote. Wanawake wa machame wanaitwa ‘Wapalestina’… Mume ukitajirika mkeo anakuua ili arithi mali.

  5. WAURU; hawa hupenda kusoma sana lakini hawapendi maendeleo kabisa. Hadi leo eneo lao la Kishumundu linatumika ku-identify wachagga washamba. Wanawake wakifikisha umri wa miaka 40 hua wehu na wanaume huwa vichaa mapema zaidi. Wanaume ni wavivu, lakini wanawake ni wachapakazi hodari. Wanazurura mjini na mabeseni wakiuza ndizi mbivu… Ukioa Uru jiandae kulea kichaa.

  6. WASIHA; Kwanza hawapendi kuitwa Wachagga. Wanajiita watu wa West-Kilimanjaro. Ni mchanganyiko wa Wachagga na WaMeru. Hawapendi shule ila wanapenda zaidi kazi za ufundi na kilimo. Viazi vingi vya Chips Arusha na Moshi vinatoka kwao. Wanawake zao wana “vigimbi” mguuni sababu ya kulima mno.!

  7. WAKIRUA; wanapenda sifa kama Wahaya. Wanawake wa Kirua ni wachawi kupindukia… Wanaloga hata jiwe ili tu alikomoe… Wanaume wa Kirua hawapendi kuoa kwao… Hawapendi kuishi mjini maana wanaogopa gharama… lakini siku wakija mjini wawili tu utadhani wako mia.

  8. WA OLD-MOSHI; Hawa ni mafundi stadi wa ujenzi wa nyumba, japo hawajengi kwao. Mpaka leo hamna daladala ya kwenda Old-Moshi inayoanzia Moshi mjini, maana ni wabishi kulipa nauli na pesa inaishia kwenye mbege njiani. Wanaume wamezoea kutoka nyumbani saa kumi na moja alfajiri na kurudi saa sita ya usiku kwa miguu.!

aiseh hd kt wachaga wanaandamwa!

Wachaga ni noma hadi askofu kasimama kuwatete!! Dah haijawahi kutokea.

Katika kabila linalotaniwa sana nadhani wachaga wanaongoza!!

Aiseee

naona hii wiki wachaga wapo kwenye headline kwelikweli, nasea watapata tabu sana

Pesa kila mtu anaijua ila style yao ya kuipenda ndio shughuli…

Wasukuma wanaongoza maana wana watani wengi mno, nadhani Wachaga wanafuata…

mi nadhani wamakonde, mmakonde ata kabila lisilo la kitani na wamakonde, huwatania.

@MENGELENI KWETU si uje huku!!!

Kwa wamarangu umenigusa.