Waraka toka kwa Tundu Lisu

WARAKA WA TUNDU LISU
KWA WANAMABADILIKO NA WATANZANIA WOTE .
(1) Ni muhimu kutambua kwamba kipindi tunachopitia hakijawahi kuwepo katika historia ya mfumo wa vyama vingi vya siasa nchini na hata wakati wa chama kimoja.
(2) Hatujawahi kuwa utawala wa kikatili wazi wazi kama huu. Hatujawahi kuwa na utawala usioheshimu Katiba na Sheria za nchi yetu wazi wazi kama huu. Hatujawahi kuwa na utawala unaokandamiza haki za binadamu na haki za kisiasa kama huu.
(3) Hatujawahi kuwa na utawala uliojiapiza wazi wazi kuwa utaangamiza vyama vya upinzani kama huu. Kutekeleza kiapo chake hicho, baadhi ya mbinu anazotumia Magufuli na watu wake ni hizi:
(a) Kukandamiza wapinzani thru mauaji, kuwapiga na kuwaumiza, kuwafunga kwa kesi za kubambikiza;
(b) Kuwarubuni kwa rushwa ya fedha au ya madaraka wale wote wanaoweza kurubuniwa;
(c) Kuwashindisha kwa nguvu wagombea wa CCM katika chaguzi za marudio.
(4) Magufuli na watu wake wanafanya yote haya kwa sababu wanajua kwamba upinzani dhidi ya CCM ni mkubwa na una nguvu kuliko pengine tunavyojifahamu sisi wenyewe. Ya 2015 yamewatisha sana na hawako tayari kuyaona tena 2020. Ndio maana ya yote haya yanayoendelea.
(5) Tufanyeje???
(a) Tuyaelewe mazingira haya mapya ya kisiasa na sababu zake kama nilivyoelezea hapo juu;
(b) Tujielewe sisi wenyewe. Chama chetu kimekuwa kikubwa sana na hivyo kimeingiza watu wa kila aina:
(i) Wapo ambao wameingia kwenye chama kwa sababu wanaamini katika haja ya kulikomboa taifa letu na kujenga mfumo bora zaidi wa kikatiba na kiutawala. Hawa tutakuwa nao katika milima na mabonde tutakayopitia kwenye safari ya ukombozi;
(ii) Wapo walioingia ili kupata madaraka ya udiwani au ubunge au Urais au mengineyo. Wamegundua kwamba maisha ya upinzani ni magumu na ya hatari sana. Hawa sio wetu na hatutaweza kuwazuia kununuliwa au kuondoka kwa hiari yao wenyewe.
(iii) Wapo walioingia kwa sababu halali kabisa lakini kwa imani kwamba safari ya ukombozi itakuwa fupi na rahisi. Wamegundua katikati ya safari kwamba njia ya ukombozi ni ndefu na imejaa miba na mawe na kila aina ya ugumu.
Wapo watakaokimbia sio kwa sababu wamehongwa, bali kwa sababu ya ugumu wa safari. Na wapo watakaobaki na kuendelea na mapambano.
(iv) Wapo walioingia kwa sababu hawaoni njia nyingine yoyote ya kujikwamua na mfumo tawala uliopo. Hawa ni wetu vile vile through thick and thin, lakini tuhakikishe hawakatishwi tamaa na haya yanayoendelea.
(v) Wapo waliopandikizwa ili watuhujumu kwa ndani. Hawa nao sio wetu na hatuwezi kuwazuia kujiondoa au kununuliwa.
Tunachohitaji kufanya ni kuweka utaratibu bora zaidi wa kuchuja kila anayeingia kwenye chama chetu; na hasa kila anayetaka au anayepewa dhamana ya uongozi wa chama wa nafasi za kiserikali kama madiwani na wabunge.
(c) Tuhakikishe chama chetu kinaendelea kuwa salama. Tusije tukafanya jambo lolote litakalompa Magufuli na watu wake sababu ya kukipiga marufuku chama chetu.
Hii haina maana tusiendelee kupigania haki na demokrasia katika nchi yetu. Ina maana tu kwamba tusifanye yale ambayo Sheria na Katiba ya nchi kwa sasa imeyakataza.
Tufanye yale ambayo Sheria na Katiba zimeyaruhusu na ni mengi. Matope ya kukiuka Katiba na Sheria za nchi yetu yabakie kwa Magufuli na watu wake, yasihamishiwe kwetu.
(d) Tuwalinde viongozi na wanachama wetu dhidi ya maonevu wanayofanyiwa. Tuweke utaratibu wa kuwatetea wanapokamatwa na wanapofunguliwa mashtaka ya uongo. Utaratibu huu uwe wa nchi nzima na tuache kutegemea kila kitu kifanywe na Makao Makuu ya chama.
(e) Tuendelee kujitolea kufanya kazi za chama. Hatuna mjomba au shangazi wa kututatulia matatizo yetu bali sisi wenyewe. Tuache kunyoosha vidole vya lawama kwa viongozi wakati sisi wenyewe hatutimizi wajibu wetu.
(f) Tujifunze kuwa na nidhamu ndani na nje ya Chama. Tuna migogoro mingi ya bure kabisa; tuna vichuki na vijiwivu visivyokuwa na msingi. Tuna vitabia vibaya vya kufikiria kwamba kila kitu lazima kitolewe nje hadharani na kujadiliwa as if hakuna taratibu za kichama za kuyajadili na kuyatatua. Lazima tuwe na nidhamu.
(g) Tuache visingizio na tufanye kazi za chama kwa bidii na maarifa. Kuna mengi ambayo yanatufanya tushindwe chaguzi kwa sababu zetu wenyewe. Haya tuyatambue na kuyarekebisha, kabla hatujakabiliana na ya Magufuli na watu wake na ya kimfumo.
Mwisho, Magufuli na watu wake wanajua hawana jawabu la matatizo ya kimsingi ya nchi yetu na ya watu wetu.
Wanataka kutuharibu ili kusiwe na sauti mbadala itakayowaambia wananchi kwamba Magufuli ameshindwa.
Tutambue kwamba vita dhidi ya CHADEMA na vyama vya upinzani ni sehemu tu ya vita kubwa dhidi ya Watanzania.
CHADEMA iko mstari wa mbele wa vita hii. Tukishindwa sisi hakuna mwingine atakayeweza kusimama na kupigana na utawala huu.
Tuna wajibu mkubwa sana.
https://scontent.fnbo1-1.fna.fbcdn.net/v/t1.0-9/39026789_574536509627780_8147125744410034176_n.jpg?_nc_cat=0&oh=95bd41569c2e758a1c95627222f4d798&oe=5BF3807B

Ni kweli Kamanda wa kweli! Ni kweli huyu fisi anavizia sasa ili auifute chadema! Huyu fisi hatashiba damu ya wapinzani hadi awamalize. Huyu fisi mwenye njaa anahangaika kila kona kwa sababu anajua 2015 tulimpiga. Na asipoiba tutampiga tena na tena!! Fisi mchafu! huyu anawinda hata mwandishi wa sasa hivi. Huyu fisi wanasheria wakiungana dhidi yake hata kama atatoa maagizo mahakamani! itakuwaje. Fatma ana kesi ya kikatiba tunahitaji kutambua viongozi wa mahakama wazalendo waliobaki kutenda haki! Bila hivyo huyu fisi atatumaliza

Nunda mla watu! Jiwe Nunda mla watu. Maaskofu wamenyamaza, masheikh wamenyamaza, mapadre wamenyamaza, > Mponye Lisu Mungu wa haki!

Hongera Tundu Lisu

Ni ukweli mtupu… ila ngoja tuone…

Cc: @Mahondaw