Kiswahili endelevu

kwa muktadha Wa kibiashara, import Na export zaitwaje

Nina swali moja mwalimu,
Wheelbarrow yaitwaje kwa kiswahili?

toroli au rukwama

1 Like

Asante, toroli nikaa imetoka kwa trolley, rukwama nimeskia Leo

2 Likes

niliambiwa hata pia mkokoteni unafaa kuitwa rukwama, basically any type of cart can be a toroli or rukwama

2 Likes

Ni kweli. Hata ‘handcart’ huitwa rukwama na siyo ‘mkokoteni’ kama tunavyojua katika lugha ya kawaida.

1 Like

[ATTACH=full]73600[/ATTACH]

@xuma ndio hayo majibu… Hangover imeniwekelea kidole pabaya

4 Likes

[U][B]
MAJIBU

ZOEZI
Nyambua maneno yafuatayo katika hali zote tano.[/B][/U]
[B]-Kula-Kuliwa,kulwa,kulia,kulana.
-Kunywa-Kunywiwa,Kunywa,Kunywia/kunywea,kunywiana/kunyweana
-Piga-Pigiwa, Pigwa, Pigia, Pigana.
-Pika-Pikiwa, Pikwa, Pikia, Pikiana.
-Lala-Laliwa, Lazwa, Lalia, Laliana.
-Tembea-Tembelewa, Tembezwa, Tembelea, Tembeleana.
-Ingiza-Ingiziwa, Ingizwa, Ingizia, Ingizana.
-Andika-Andikiwa, Andikwa, Andikia, Andikiana.
-Tega-Tegewa, Tegwa, Tegea, Tegana.
-Lia-Liliwa, Lizwa, Lilia, Lizana.
-Bana-Baniwa, Banwa, Bania, Baniana.
-Kaza-Kaziwa, Kazwa, Kazia, Kazana.

Kongole kwa kina @Mjuaji , @Okwonkwo , @123tokambio , @introvert , @Eng’iti , @Meria Mata , kwa juhudi zenu. @Yule Karis Black hata nawe kongole kwa kushiriki. @Eng’iti , @Mjuaji na @Okwonkwo wamezoa alama za juu kenye hili zoezi.

Tunapolala tukumbuke kuwa ‘tusilolijua ni usiku wa giza tu’.

Alamsiki![/B]

5 Likes

:D:D:D:D:DUbunifu wako umenichekesha. Hata hivyo umejaribu sana.

1 Like