Naitwa New Villager....

Jamaniiii, hapa nishavuta kumbukumbu hadi masikio yanaenda upande… nakumbuka ofa ya mwisho nilipewa ilikuwa kwenda kufuturu, na ile ofa niliikubalia. Je ndo hiyo? ni wewe maana hapa uko na jina jipya sijajua kule JF ulikuwa unatumia jina gani.

Sikukumbikia jamanii, nilikukubalia ila nikawa nasubiri maelekezo ya eneo husika ni wapi… sikuona PM wala maelezo zaidi nikawa mpole.

Sijui ofa bado ipoo…:confused:

Hahahahaaaaaaa

Hapo sasa umepata sifa ya kuteuliwa kuwa mjumbe kwenye kamati ya uongozi ya nyumba kumi

Kassiee…mi natangaza ndoa huku ughaibuni tunaifungia palee moi kasarani…angalau hii mbaridi ya hapa Nairobi ipite kuleee…

Hivo eeeh, basi itabidi niokae macho uchaguzi au uteuzi ukianza tuu nujitokeze nami nichaguliwe niwe balozi kabisa kama sio katibu tarafa au katibu kata hahahahha.

Nice to meet you here…

Hakiya

Haki ya Mungu ukiwa na mwanamke mwenye kumbukumbu kama kassie huna haja ya kuwa na kompyuta…haswaa ndiyo ile futari…nikawa bize kuwasiliana na waandari wa ile futari kurudi tayari tushawekewa mapadiloku…nilipoingia nilikuta notifications tu sikuweza kuzisoma tena…anyway kesho…nasema kesho…ukuje hapa karipu na afisi ya gavana wa hii county ya nbi tusherehekee eid pamoja na mafriends zangu pia unawesa kuja na mafriends sako.

Kilichonifurahisha zaidi hawa Wakenya wametutangazia hadi kwenye The citizen kama jinis tulivyohamia huku

Sikuwa na imani kama tungekutana tena wana villager wa JF

Toobaaah… nifinye basi sikio nawolewa na nani!!! Ila ujiandae kuvumilia hehehehee

Hahahahahahah lol ngoja nipambane na hali yangu

Hhehehehehehe kwahiyoooo, kwakifupi ni kuwa unaandaa pati ya kusherehekea Eid… na mie ni mmoja wa waalikwa…

Basi Inshallah, panapo maajaaliwa Eid pili ntakuwa available. Nimekuja nyumbani mara moja, ule msiba wa wanafunzi wa chuo waliopata ajali wkenye ambulance mmoja wapo ni binamu yangu. Hivo kesho siku ya Eid ntakuwa msibani ila jumamosi nipo na jumapili nageuza kurudi kazini. Count me in on Saturday.

Napenda wanawake wajanja wajanja ili angalau wanifanye nifiri zaidi.

Nimefurahi kukuona huku. Nilikuwa najiuliza nitakujulishaje uhamie kipande hii

Hhahahahaaaa sawa mwanakijiji mwenzangu, pongezi na shukrani tuzipeleke kwa jirani zetu wakenya kwa kutusitiri. Japo nguo ya kuazima huwa haisitiri…:stuck_out_tongue:

Pambana ndugu yangu, mapambano ndo yameanza hivo hakuna kulaza damu. Ni mwendo wa mchaka mchaka hadi Mzee Baba nae atu join kwenye hii jogging hahahahaa.

Ila Bongo nyoso

Sijui wakenya wanaliitaje jibu kwa kiswahili chao:p:p:p:p:p

Haya soina hiyana mie, karibuuu.

Kasie Mahaba Matata.

Nashukuru kuniwaza, nimefika mwenyewe tuu, ila nimefikaje fikaje hata sielewi…

Oooh poleni sana…wape pole ukweni huko…ooh yaeh I saw that picture taken on the scene… Dah so sad…
Party ni nzuri kwa kujiliwaza na kuongeza network… J3 ukinikuta kny tractor shambani utadhani siyo Mimi…

Hhahahahahhaa hivi huku nako kuna BAN…???

Itakuwa jibu lake wamaliita makaliole… ahahahahahahaa

Asanate sana, nashukuru tushapoa. Yeah party inaongeza urefu wa maisha maana inakuweka mbali namaswahibu ya dunia hii.

Jumatatu utakuwa shambani??!!!, shamba lako liko wapi nion kama naweza pata ruhusa ya kuja kujaribu kulima?