Ntolilo ila JF ya mwanzo kulikuwa na ustaarabu mkubwa sana watu walishindana kwa nguvu ya hoja bila kuitana haya mshenzi au mpumbavu.
Tatizo lilianza pale MACCM walipostuka na kuanza kuiona JF ni tishio kwa hoja zilikuwa zikijengwa za maovu yao mbali mbali hasa ufisadi na pia waliona kwamba idadi ya wanachama ilikuwa inakuwa kwa kasi.
Yule Mwigulu katika kikao kimoja cha MACCM akaweza kuwashawishi MACCM kuweka bajeti ya kuwalipa buku 7 na pia kuwapa laptop kuja humu ili kuvuruga mijadala kwa namna yoyote ile ikiwemo kutumia matusi ya nguoni.
Walipoingia tu ndiyo tatizo la urushaji matusi likashamiri sana. Buku 7 hawakujali kufungiwa kwani walikuwa wana IDs chungu nzima hivyo kufungiwa kwao hakukuwa tatizo kwani ikifungiwa ID moja anahamia nyingine na kuendelea kurusha matusi. Walikuwa hawana hoja zenye nguvu kwani ni kazi mno kujenga kuwa na hoja nzito huku reality ikionyesha MACCM na Serikali yao yananuka rushwa na ufisadi uliokithiri.
Duh JF ikageuka kiwanda cha ajira aiseee. Hapo hapo imetumika nguvu kubwa kuua hizo ajira sijui wahusika wanajisikiaje huko walipo kwa kukosa pesa za bure
Naam kun awatu ambao labda kwa sasa hawana ajira kisa dikteta kutotaka kukosolewa kwa maovu yake mbali mbali. Na si ajira za JF tu bali blogs nyingi nyingine ambazo hawakuweza kumudu masharti makubwa ya kujiandikisha hasa kutokana na bei kubwa.