Mwalimu Xuma Karejelea kijiji chake!

Baada ya muda usiopimika,
Baada ya kuzuru sehemu mbalimbali kwenye ulimwengu huno,
Baada ya kutaadhmini na kuyastaajabia mandhari tofauti,tofauti,
Baada ya kuzikabili kimasomaso shughuli zilizobidi,
Baada ya kuimarisha ngome yangu ya lugha ya kiswahili kwa kuongeza ufasaha, ufahamu na umaahiri,
Baada ya kupigwa butwaa na lugha ilivyoborongwa na wale wa ’ yaliyondwele sipite’,
Mimi ndiye huyo Mwalimu nabisha tena kwa moyo mkunjuuufu…hodi hodi ‘tumesija’.
Salamu za dhati kwa ndugu zangu kina @123tokambio ,@The_Virus , @Meria Mata , @gashwin , @Mjuaji , @vincelly , @admin , @Mkufuu , @bababibitoto , @coldpilsner na wengineo wapenzi wa lugha. Kwa wageni waliojiunga nasi, dumisha umakinifu wa lugha! Na siyo tafadhali!

'Mwenda tezi na omo, marejeo no ngamani. Kijiji ni ‘ngamani’!

9 Likes

Sijui kwa nini naskia tu ku-derail hii thread. This village offers various eye cleansing services.Whats your take on this?
[ATTACH=full]119555[/ATTACH]

2 Likes

Umederail ya @burjuman tukiona,hauogopi kutumiwa special forces huko bulbul?

Ni ‘kutathmini’ sio ‘taadhmini’.

1 Like

Hehe. Acha nicheze chini

3 Likes

Tathmini. Kubofya vidufe kwa haraka kakangu.

7 Likes

Karibu Mwalimu @xuma
Shukran kwa kumaliza masomo

1 Like

Yastahili kaka.

Yaliyo ndwele sipite.

Karibu gwiji.

1 Like

Shukran kaka mkubwa. Naona umetunukiwa taji la ‘Mdhamana was Kijiji’ yaani ‘village sponsor’!

1 Like

Shukrani teletele.

Alipata juu ya umama.
Mwalimu unaweza tupa ngano moja ya ulipokuwa na iwe na thresholdi?

3 Likes

Kuderail natumai ni kulipua kwa kiswahili

1 Like

Ngano yaja.

thresholdi ndio gani?
Unakaa wewe ni mlemavu wa lugha.

1 Like

@Meria Mata anachosema kina ukweli?

Threshold.……kingo kwa kiswahili. Kuashiria ‘mwisho’.

1 Like

Karibu tena mwalimu, tulikukosa.

1 Like

Nimonimo.Tupotupo!

1 Like

sand sana, lakini sisi kama wapenzi wa lugha…

1 Like