Wakimbizi wa mtandaoni!!

Yale mambo yaliyotufanya tuwapokee wakimbizi toka nchi jirani ndiyo yametufanya na sisi tuwe wakimbizi wa mtandaoni. Tumo Kambini tunapewa msaada unaotuwezesha kuishi angalau kama binadamu mtandaoni. Asante Kenyatalk kwa kutufadhili!

Tunajiita “Diaspora”

Hii ni aibu kubwa sana kwa nchi yetu

Awamu ya 5 chini ya kiongozi jiwe ameleta utumwa wa aina yake kabisa

Hivi JF ndio mekufa? Naona umehama na jina lako, unafanyaje>

Tumekuwa wakimbizi ghafla

Kisiwa cha Amani ati8i

Jf haijafa mkuu ndio wako kwenye harakari za kuirejesha hewani, ila sijui kama itakujakuwa huru kama awali

Sijahama na jina mkuu, ila nimesajili id ile ile ilioko jf tz

Nimekupata, kweli tumekuwa wakimbizi, tumekimbia kwetu JF na kuja Kenya talk. Nina imani JF watarudi tu! JF ni maisha ya watu, kuna watu mkate wao ni JF.

Basi ngoja nami nisajiri ID yangu!

Inasikitisha sana…

Ni sawa na kutokua na uhuru au kauli mbele ya baba yake, kwa hiyo matatizo yako yote unaenda kuyasemea kwa baba wa jirani…

Hii inapelekea jirani kutambua udhaifu wa baba yako na namna gani ya kumvuruga…

Cc: @Mahondaw

Kurudi itarudi kikubwa tuwe wavumilivu tu

Wakimbizi oyeeeee!! mko nchi jirani kwa sasa mmekimbilia kisiasa

Uvumilivu ukizidi hata mbivu unaeza kuta zimeharibika ushindwe kuzila.

Ni kweli lakini tujitahidi tu kuvumilia

sisi ni watu wa kuvumilia tu. hata Melo nae huko aliko anavumilia. Acha nile Githeri akili ikae sawa

Karibu sana mkuu.

Siku zote Plan B ni muhimu katika kufanya jambo

Njoo tukutane hapa F2000 mkuu, japo ni pa kizamani ila upande huu wa stripplers utatufaa

Ni wapi huko mkuu?

Hapa Nairobi karibu na ilipp Kencom