Huyu dada yako ndiye mkubwa kwenu, tangu ukiwa mdogo alikuogesha, alikufulia, alikufundisha kupika. Ulipoanza shule yeye alishamaliza lakini kwakua ulisoma shule aliyosoma yeye, aliomba aliowaacha wakuangalie.
Dada ameolewa, mume wake alikununulia kiwanja kwa ahadi usimwambie dada yako. Juzi shemeji amesema hataki upate shida ya kwenda kazini na mabasi, ameamua kukununulia Jimmy Choo, lakini pia anakwambia usimwambie dada. Huyu dada wewe unamuona kama mama yako, hutaki kumuudhi lakini dada anampenda mume wake balaa.
Likikufika utalitatuaje na wewe unakaa huku kwetu Kwamtogole, kiwanja umepatiwa Chanika na unatamani ujenge ili uhame.
Ukianza kudanganya uongo mmoja utaendelea kudanganya ili kuulinda uongo uliotangulia. Hapo ukiendekeza tamaa tu lazima uliwe, na unauweka uhusiano wa pande zote tatu katika majaribu mazito sana, chukua hatua ya maamuzi ya ama kukataa au kukubali from the very beginning
Kukataa nakubaliana nawe Shunie lakini kumwambia dadako hapana, waweza haribu ndoa na maisha ya huyo sis wako na familia yake. You just be strong, ushinde moyo wako na tamaa navishawishi vye fedha na ahadi za kupewa good time na umkabili shem kwa msimamo ulio thabit, atakuomba radhi nakwambia
Hmm! Kama yote hayo uliyofanyiwa na shemeji hukuwahi kumwambia dada’ako, sasa unaanzaje kumwambia baada ya kutakiwa kulipa fadhila! Au ulidhani hivyo vitu ulikuwa unapewa kiushemeji (hisani)?.. :D:D:D
Dhambi ya uzinzi si lazima hadi mfanye tendo, hata kutamani asiye mume wako (kupewa vitu na ukaambiwa usimwambie dada yako na wewe ukakubaliana na hali hiyo) ni uzinzi…